Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: Kuanzia kwenye mupaka wa kaskazini kwenye barabara ya Hetiloni mpaka kuingia Hamati hata Hazorenoni unaokuwa katika Damasiki na Hamati upande wa kaskazini na kuendelea kutoka mashariki mpaka magaribi. Eneo hilo litakuwa la kabila la Dani.
Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.
Eneo la inchi yao lilikuwa na miji ya: Zora, Estaoli, Iri-Semesi, Salabinu, Ayaloni, Itila, Eloni, Timuna, Ekuroni, Elteke, Gibetoni, Balati, Yehudi, Bene-Beraki, Gati-Rimoni, Me-Yarkoni na Rakoni na inchi iliyokuwa karibu na Yopa.
Katika siku zile hakukukuwa mufalme katika Israeli. Basi kabila la Dani lilikuwa linatafuta eneo lake lenyewe la kuishi ndani yake, maana mpaka wakati ule, halikukuwa limegawanyiwa sehemu yake lenyewe kati ya makabila ya Israeli.