hata eneo la inchi yao likakuwa toka Sidona kuelekea upande wa kusini, kuendelea Gerari mpaka Gaza, na kuelekea upande wa mashariki liliendelea kwa Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu mpaka Lasa.
Umefezeheka, ewe Sidona, muji wenye upango kandokando ya bahari! Bahari yenyewe inatangaza: Sijapata kuwa na uchungu wa kuzaa, wala sijazaa; sikulea vijana wanaume, wala kukomalisha wabinti!
Basi Yesu akarudi tena Galilaya katika muji Kana, pahali alipogeuza maji kuwa divai. Kule kulikuwa mukubwa mumoja wa serikali, aliyekuwa na mwana mugonjwa katika muji Kapernaumu.
Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.
Wakaaji wa muji ule hawakukuwa na mutu wa kuwaokoa kwa sababu walikuwa mbali na muji wa Sidona, tena hawakukuwa na ushirika na watu wengine. Muji ule ulikuwa kwenye bonde la Beti-Rehobu. Watu wa kabila la Dani wakaujenga upya, wakaishi mule.