Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 19:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Alameleki, Amadi na Misali. Kwa upande wa magaribi mupaka uligusana na Karmeli na Sihori-Libunati.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 19:26
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa, uwakusanye watu wote wa Israeli mbele yangu kule kwenye mulima Karmeli. Vilevile, uwakusanye wale manabii mia ine na makumi tano wa Bali, na manabii mia ine wa Ashera ambao wanakulishwa na malkia Yezebeli.”


Basi, Ahabu akawaita watu wote wa Israeli, akawakusanya na manabii wote kule kwenye mulima Karmeli.


Basi, Ahabu akaenda zake kula na kunywa. Naye Elia akapanda juu ya kilele cha mulima Karmeli, na kule akainama uso mpaka chini na kuuweka uso wake katikati ya magoti yake.


Elisha akaendelea na safari yake mpaka kwenye mulima Karmeli na tokea kule akarudi Samaria.


Shingo yako ni kama munara wa pembe za tembo. Macho yako ni kama visima vya muji wa Hesiboni, karibu na mulango wa Beti-Rabi. Pua yako ni kama munara wa Lebanoni, ambao unauelekea muji wa Damasiki.


Inchi inaomboleza na kunyauka; pori ya Lebanoni imekauka, bonde zuri la Saroni limekuwa jangwa, kule Basani na mulima Karmeli majani yote yamekauka.


Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.


Umewatuma watumishi wako kumuchekelea Bwana wenu; wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita, nimefika juu kwenye vichwa vya milima, mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni. Nimeangusha mierezi yake mirefu, na misunobari mizurimizuri. Nimevifikia vichwa vyake na ndani ya pori zake kubwa.


Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi– kweli adui anakuja kuwashambulia: ni hakika kama vile Tabori unavyokuwa mulima, kama vile mulima Karmeli unavyoonekana kutoka katika bahari.


Eneo la inchi yao lilikuwa na miji ya: Helkati, Hali, Beteni, Akisafu,


Kisha ukageuka kuelekea mashariki kwenda Beti-Dagoni ambako unagusana na Zebuluni na bonde la Ifitaheli. Halafu ukaendelea kaskazini ukafika Beti-Emeki, Neieli na kuzidi kuelekea kaskazini ukafika Kabuli,


Katika eneo la kabila la Aseri walipewa Misali pamoja na mbuga zake za malisho, Abudoni pamoja na mbuga zake za malisho,


Samweli alisikia kwamba Saulo alikuwa amekwenda kule Karmeli na amesimamisha munara wa ukumbusho wake, na kwamba amekwenda Gilgali. Hivyo, kesho yake, Samweli aliamuka asubui mapema, akaenda kukutana na Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ