Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 19:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18-22 Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya: Yezereheli, Kesuloti, Sunemu, Hafaraimu, Sioni, Anaharati, Rabiti, Kisioni, Ebesi, Remeti, Eni-Ganimu, Eni-Hada na Beti-Pasesi. Vilevile, mupaka wao ulifika Tabori, Sahasuma, Beti-Semesi na kuishia kwenye muto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 19:18
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kule, Abeneri akamusimika Isiboseti kuwa mufalme wa inchi ya Gileadi, Asheri, Yezereheli, Efuraimu na Benjamina na Israeli yote.


Basi, wakatafutatafuta binti muzuri katika inchi yote ya Israeli. Kukapatikana binti mumoja muzuri anayeitwa Abisagi Musunami. Wakamuleta kwa mufalme.


Naye akasema: “Tafazali, ninakusihi umwombe mufalme Solomono aniruhusu nimukamate Abisagi, yule Musunami, akuwe muke wangu, kwa maana ninajua hatakukatalia wewe.”


Naye akasema: “Umuruhusu ndugu yako Adonia amwoe Abisagi, yule Musunami.”


Nyuma ya mambo hayo, Naboti wa muji wa Yezereheli alikuwa na shamba lake la mizabibu kule Yezereheli, karibu na nyumba ya Ahabu, mufalme wa Samaria.


Akamwambia mutumishi wake Gehazi: “Umwite yule mama Musunami.” Alipomwita akakuja na kusimama mbele yake.


Siku moja Elisha alikwenda Sunemu, ambako kulikuwa mama mumoja tajiri. Mama yule akamwalika Elisha kwa chakula, na toka siku hiyo ikakuwa kawaida Elisha kula chakula kwake kila mara alipopitia kule.


Kisha mufalme Yoramu akarudi katika muji Yezereheli kusudi apate kutunzwa vidonda alivyoumizwa na Waaramu kule Rama, alipopigana na Hazaeli mufalme wa Aramu. Naye Ahazia mwana wa Yehoramu, mufalme wa Yuda alimwendea Yoramu mwana wa Ahabu kule Yezereheli, kwa sababu alikuwa mugonjwa.


Lakini mufalme Yoramu alikuwa amerudi Yezereheli kusudi apate kutunzwa vidonda alivyopata wakati wa kupigana katika vita na mufalme Hazaeli wa Aramu. Yehu aliwaambia wakubwa wenzake: “Ikiwa mutakubaliana nami, mutu yeyote asitoke Ramoti kwenda Yezereheli kwa kupeleka habari hizi.”


Yehu alipofika Yezereheli, Yezebeli alikuwa amekwisha kupata habari ya mambo yaliyotokea. Alijipakaa rangi kwenye macho na kuchanua nywele zake, kisha akaenda kwenye dirisha na kuangalia chini.


Nao wakamujibu: “Ni kweli kwamba inchi hii ya milima haitutoshi. Hata hivyo wale Wakanana wote wanaokaa kwenye bonde wana magari ya chuma, vilevile wale wote wanaokaa Beti-Seani pamoja na vijiji vyake, na wale wanaoishi katika Bonde la Yezereheli.”


Kura ya ine ilizipata ukoo za kabila la Isakari.


Wafilistini walikusanyika na kupiga kambi yao kule Sunemi; na Saulo aliwakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao kwenye mulima Gilboa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ