Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumutumikia Yawe. Gadi, Rubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha kupata sehemu yao upande wa mashariki wa muto Yordani. Walipewa sehemu hii na Musa, mutumishi wa Yawe.”
Basi, watu hao wakaanza safari ya kwenda kuichunguza inchi. Mbele hawajakwenda, Yoshua akawapa maagizo: “Muende katika inchi yote muandike maelezo kamili juu ya hiyo inchi, kisha murudie kunielezea, nami nitapiga kura mbele ya Yawe hapahapa Shilo juu ya sehemu mutakayopewa.”