Karibu na saa kumi na moja akatoka tena, naye akakuta watu wengine wakisimama pale kwenye nafasi ile. Akawauliza: ‘Sababu gani munasimama bure hapa muchana kutwa?’
Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”
Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.
Wao wakasema: “Musimame tuende na kuishambulia inchi hiyo. Tumeiona na kweli ni inchi yenye mboleo. Mutakaa hapa tu bila kufanya kitu? Musikawie kwenda kuirizi inchi hiyo.