Kule, mupaka uligeuka kwenda kaskazini kuelekea Eni-Semesi, ukapitia Geliloti karibu na mwinuko wa Adumimu na kuteremuka mpaka kwenye jiwe la Bohani mwana wa Rubeni.
Tena, ukaendelea kwa upande wa kaskazini wa kilima cha Beti-Hogla na kuishia kaskazini kabisa ya guba ya bahari ya Chumvi, pahali muto Yordani unapoingilia. Huu ni mupaka wake kwa upande wa kusini.