Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 17:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Eneo la kabila la Manase lilianzia Aseri na kwenda hata Mikimetati upande wa mashariki ya Sekemu; halafu mupaka wao ukaendelea upande wa kusini mpaka kwenye inchi ya wakaaji wa Eni-Tapua.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 17:7
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Sekemu mwana wa Hamori Muhivi, aliyekuwa mukubwa wa inchi hiyo, alipomwona Dina, akamushika, akalala naye kwa nguvu.


Siku moja, wandugu za Yosefu wakakwenda kuchunga nyama wa baba yao karibu na Sekemu.


Baba yake akamwambia: “Kwenda uwaangalie wandugu zako na nyama kama wako salama, kisha uniletee habari.” Basi, Yakobo akamutuma Yosefu kutoka bonde la Hebroni. Yosefu alipokaribia Sekemu,


Basi, Rehoboamu akaenda Sekemu ambako Waisraeli wote walikuwa wamekusanyika kwa kumuweka kuwa mufalme.


Nyuma ya mambo hayo, mufalme Yeroboamu akaujenga upya muji wa Sekemu kwenye mulima wa Efuraimu. Akakaa kule. Kisha akaenda kujenga muji wa Penueli.


Uwaarifu kwa vitambulisho wale wanaokuheshimu, wapate kuuepuka mushale.


kwa sababu wabinti wa Manase waligawanyiwa sehemu zao kama vile wanaume wa kabila lao walivyogawanyiwa. (Wazao wengine wa Manase walipewa inchi ya Gileadi.)


Inchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini muji wa Tapua, ambao ulikuwa kwenye mupaka, ulikuwa mali ya wazao wa Efuraimu.


Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.


Walipewa Sekemu, muji ambao ulikuwa vilevile muji wa kukimbilia usalama, pamoja na mbuga zake za malisho katika inchi ya milima ya Efuraimu, na Gezeri pamoja na mbuga zake za malisho,


Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu.


Mifupa ya Yosefu ambayo Waisraeli walikuwa wameileta kutoka Misri waliizika kule Sekemu katika eneo ambalo Yakobo alikuwa amelinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba ya Sekemu, kwa bei ya vikoroti mia moja vya feza. Eneo lile nalo likakuwa mali yao wazao wa Yosefu.


Abimeleki mwana wa Gideoni, akawaendea wandugu na wana wote wa kabila za mama yake kule Sekemu, akawaambia:


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ