Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 17:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 lakini tena inchi ya milima itakuwa yenu. Ingawa sasa ni pori, mutaifyeka na kuirizi yote toka upande huu mpaka upande mwingine. Mutawaondoa Wakanana, hata kama wana magari ya chuma na ni wenye nguvu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 17:18
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini upinde wake bado imara, na mikono yake imepewa nguvu, kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo, kwa jina la Muchungaji, Mulinzi wa Israeli.


Kwa hiyo, waaskari wa Daudi wakaenda katika mbuga kwa kupigana na watu wa Israeli. Mapigano hayo yalifanyika katika pori la Efuraimu.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda.


Utukufu wake ni utukufu wa ngombe dume wa kwanza, pembe zake ni za mbogo dume. Atazitumia kusukuma mataifa; yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia. Efuraimu atakuwa na pembe hizo elfu kumi na Manase kwa maelfu.”


Kwa sababu hii tunaweza kusema kwa uhodari: “Bwana ndiye musaidizi wangu; sitaogopa kitu. Mwanadamu ataweza kunifanya nini?”


vilevile eneo la milima inayokuwa kati ya Lebanoni na Misirepoti-Maimu ambayo wakaaji wake ni Wasidoni. Kadiri na jinsi Waisraeli watakavyoendelea mbele, mimi mwenyewe nitayafukuza mataifa hayo katika inchi hizo mbele yao. Nawe utawagawanyia Waisraeli sehemu mbalimbali za inchi hizo kwa kura kama nilivyokuamuru.


Kutoka hapo, ulielekea kwenye mulima mpaka chemichemi za Nefutoa, mpaka kwenye miji ya mulima wa Efuroni. Hapo mupaka uligeuka na kuelekea Bala, ni kusema Kiriati-Yearimu,


Basi, Yoshua akawaambia wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Efuraimu na Manase: “Kweli ninyi mumekuwa wengi na wenye uwezo mukubwa. Haifai mupate sehemu moja tu,


Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.


Kulikuwa mutu mumoja katika muji wa Rama katika inchi ya milima ya Efuraimu jina lake Elekana wa kabila la Efuraimu. Yeye alikuwa mwana wa Yerohamu, na mujukuu wa Elihu mwana wa Tohu mwana wa Zufu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ