Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 17:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Nao wakamujibu: “Ni kweli kwamba inchi hii ya milima haitutoshi. Hata hivyo wale Wakanana wote wanaokaa kwenye bonde wana magari ya chuma, vilevile wale wote wanaokaa Beti-Seani pamoja na vijiji vyake, na wale wanaoishi katika Bonde la Yezereheli.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 17:16
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya wakati kidogo mbingu zikatanda mawingu mazito, upepo ukavuma, kukanyesha mvua kubwa. Ahabu naye akapanda ndani ya gari lake la vita, akarudia Yezereheli.


Nguvu ya Yawe ikamufikia Elia, naye akajitayarisha kusafiri, akakimbia na kumutangulia Ahabu kuingia ndani ya muji Yezereheli.


Nyuma ya mambo hayo, Naboti wa muji wa Yezereheli alikuwa na shamba lake la mizabibu kule Yezereheli, karibu na nyumba ya Ahabu, mufalme wa Samaria.


Tena, Yawe anasema hivi juu ya Yezebeli: ‘Imbwa wataukula mwili wa Yezebeli humuhumu katika muji wa Yezereheli.


Yezebeli hatazikwa na mutu. Maiti yake itakuliwa na imbwa katika inchi ya Yezereheli.’ ” Kisha kusema hayo, nabii akaondoka ndani ya chumba na kukimbia.


Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mboleo ndani ya shamba katika inchi ya Yezereheli, hata hakuna atakayeweza kumutambua.’ ”


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitavumisha sauti ya vita juu ya Raba muji wa Waamoni. –Ni ujumbe wa Yawe.– Raba utakuwa lundo la uharibifu, vijiji vyake vitateketezwa kwa moto. Halafu Israeli atatwaa tena urizi wake. Ni Yawe anayesema hivyo.


Vilevile katika inchi ya kabila la Isakari na kabila la Aseri, kabila la Manase lilipatiwa miji ya Beti-Seani na Ibuleamu pamoja na vijiji vyake, na miji ya Dori, Eni-Dori, Tanaki na Megido pamoja na wakaaji na vijiji vyake; na sehemu moja ya tatu ya Nafati.


Yoshua akawajibu: “Kama mumekuwa wengi hivyo, hata inchi ya milima ya Efuraimu haiwatoshi tena, basi muende katika pori katika inchi ya Waperizi na ya Warefaimu, mufyeke pori hiyo na kufanya makao yenu kule.”


Basi, Yoshua akawaambia wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Efuraimu na Manase: “Kweli ninyi mumekuwa wengi na wenye uwezo mukubwa. Haifai mupate sehemu moja tu,


lakini tena inchi ya milima itakuwa yenu. Ingawa sasa ni pori, mutaifyeka na kuirizi yote toka upande huu mpaka upande mwingine. Mutawaondoa Wakanana, hata kama wana magari ya chuma na ni wenye nguvu.”


Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya: Yezereheli, Kesuloti, Sunemu, Hafaraimu, Sioni, Anaharati, Rabiti, Kisioni, Ebesi, Remeti, Eni-Ganimu, Eni-Hada na Beti-Pasesi. Vilevile, mupaka wao ulifika Tabori, Sahasuma, Beti-Semesi na kuishia kwenye muto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.


Yawe alikuwa pamoja na watu wa kabila la Yuda, nao wakaiteka inchi ya milima. Lakini hawakuweza kuwashinda wenyeji wa inchi ya bonde kwa sababu magari yao ya vita yalikuwa ya chuma.


akakusanya waaskari wake wote na magari yake mia tisa ya chuma, akaondoka Haroseti-Hagoimu, akaenda kwenye muto Kisoni.


Mufalme Asikie alikuwa na magari ya vita mia tisa ya chuma. Aliwagandamiza sana Waisraeli kwa miaka makumi mbili; nao wakamulilia Yawe awasaidie.


Wamidiani, Waamaleki na watu wote wanaokaa pembeni ya muto Yordani wakapiga kambi zao katika bonde la Yezereheli.


Wafilistini walikusanya makundi yao yote ya waaskari kule Afeki, na Waisraeli walipiga kambi kwenye chemichemi ya bonde la Yezereheli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ