Aliona kwamba pahali pa kupumzikia ni pazuri, na kwamba inchi ni ya kupendeza, akauinamisha mugongo wake kubeba muzigo, akakuwa mutumwa kwa kufanya kazi za kinguvu.
Kulikuwa vita ya muda murefu kati ya watu waliokuwa upande wa jamaa ya Saulo, na wale waliokuwa upande wa jamaa ya Daudi. Lakini Daudi alizidi kupata nguvu zaidi na zaidi, wakati upande wa Saulo ulizidi kuwa zaifu zaidi na zaidi.
Waefuraimu hawakuwafukuza Wakanana walioishi Gezeri. Wakanana hao waliendelea kukaa kati ya watu wa Efuraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.
Watu wa kabila la Zebuluni hawakuwafukuza wakaaji wa muji wa Kitironi, wala wale wa muji wa Nahalali, waliendelea kukaa pamoja nao wakiwatumikisha kazi za kulazimishwa.
Watu wa kabila la Nafutali hawakuwafukuza wakaaji wa muji wa Beti-Semesi au wakaaji wa Beti-Anati, lakini walikaa pamoja nao. Hata hivyo wenyeji wa miji hiyo walitumikishwa kazi za kulazimishwa.
Waamori waliendelea kuishi katika miji iliyokuwa katika kilima cha Heresi, Ayaloni na Salabimu. Lakini watu wa makabila ya Manase na Efuraimu waliwatawala Waamori na kuwatumikisha kazi za kulazimishwa.