Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 17:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Vilevile katika inchi ya kabila la Isakari na kabila la Aseri, kabila la Manase lilipatiwa miji ya Beti-Seani na Ibuleamu pamoja na vijiji vyake, na miji ya Dori, Eni-Dori, Tanaki na Megido pamoja na wakaaji na vijiji vyake; na sehemu moja ya tatu ya Nafati.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 17:11
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alikwenda na kuitwaa mifupa ya Saulo na ya mwana wake Yonatani kutoka kwa wakaaji wa Yabeshi-Gileadi, waliokuwa wameiiba kutoka kule Beti-Sani, ambako Wafilistini walikuwa wamemutundika Saulo na Yonatani siku ile walipomwua Saulo kwenye mulima Gilboa.


Haya ni maelezo juu ya mufalme Solomono, jinsi alivyowatumikisha watu kazi za kulazimishwa katika kujenga nyumba ya Yawe, nyumba yake ya kifalme, uwanja wa Milo, na ukuta wa Yerusalema, na vilevile katika kujenga upya miji ya Hazori, Megido na Gezeri.


Ahazia mufalme wa Yuda alipoona yaliyotukia alikimbia akielekea Nyumba ya Bustani, naye akifuatwa na Yehu. Yehu akawaamuru watu wake: “Mumwue naye vilevile!” Nao wakamupiga mushale akiwa ndani ya gari kwenye njia ya kupandia Guri karibu na muji wa Ibuleamu. Halafu alikimbilia Megido na kufia kule.


Na vilevile kwenye mipaka ya wana wa Manase: Beti-Seani na vijiji vyake, Tanaki na vijiji vyake, Megido na vijiji vyake na Dori na vijiji vyake. Hiyo ndiyo miji ambomo wazao wa Yosefu, mwana wa Israeli walimoishi.


Lakini Yosia hakukubali kumwachilia. Akakataa kusikiliza maneno Mungu aliyosema kwa njia ya Neko, kwa hiyo akajibadilisha kusudi asitambulikane, kisha akaingia katika vita katika bonde la Megido.


Uwatendee ulivyowatendea Wamidiani, ulivyowatendea Sisera na Mufalme Asikie kwenye muto Kisoni,


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo nitavumisha sauti ya vita juu ya Raba muji wa Waamoni. –Ni ujumbe wa Yawe.– Raba utakuwa lundo la uharibifu, vijiji vyake vitateketezwa kwa moto. Halafu Israeli atatwaa tena urizi wake. Ni Yawe anayesema hivyo.


Siku hiyo kutakuwa maombolezo makubwa katika Yerusalema kama vile maombolezo ya kumwomboleza Hadadi-Rimoni katika bonde la Megido.


na kwa wafalme waliokuwa katika milima ya upande wa kaskazini, waliokuwa Araba ambayo ilikuwa upande wa kusini wa Kineroti, kwenye mabonde na waliokuwa Nafoti-Dori katika upande wa magaribi.


mufalme wa Dori katika sehemu ya Nafoti-Dori, mufalme wa Goyimu kule Gilgali na


pamoja na miji na vijiji ambavyo waliongezewa kutoka kwenye inchi ya kabila la Manase.


Eneo la kusini lilikuwa la kabila la Efuraimu na eneo la kaskazini lilikuwa la kabila la Manase, mupaka wake ukiwa bahari ya Mediteranea kwa upande wa magaribi. Kabila la Aseri lilikuwa upande wa kaskazini-magaribi wa eneo la Manase na la kaskazini-mashariki lilikuwa kabila la Isakari.


Nao wakamujibu: “Ni kweli kwamba inchi hii ya milima haitutoshi. Hata hivyo wale Wakanana wote wanaokaa kwenye bonde wana magari ya chuma, vilevile wale wote wanaokaa Beti-Seani pamoja na vijiji vyake, na wale wanaoishi katika Bonde la Yezereheli.”


Watu wa kabila la Manase hawakuwafukuza wakaaji wa miji ya Beti-Seani na vijiji vyake, Tanaki na vijiji vyake, Dori na vijiji vyake, Ibileamu na vijiji vyake, na Megido pamoja na vijiji vyake. Wakanana waliendelea kukaa kule.


“Kule Tanaki, pembeni ya chemichemi za Megido, wafalme walikuja, wakapigana; wafalme wa Kanana walipigana, lakini hawakuteka feza.


Halafu Saulo akawaambia watumishi wake: “Munitafutie mwanamuke ambaye anaweza kuaguza kusudi nimwendee na kumwomba shauri.” Watumishi wake wakamujibu: “Kuna mwanamuke mwaguzi mumoja kule Endori.”


Zile silaha zake waliziweka katika nyumba ya Astaroti. Kisha wakautundika mwili wake kwenye ukuta wa muji wa Betisani.


mashujaa wote waliondoka, wakasafiri usiku kucha, wakaondoa mwili wa Saulo na miili ya wana wake kutoka ukuta wa Betisani, wakakuja nayo mpaka Yabesi na kuiteketeza kwa moto kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ