Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 17:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watu wa kabila la Manase ambaye alikuwa muzaliwa wa kwanza wa Yosefu, vilevile walipewa eneo lao kwa kura. Makiri, muzaliwa wa kwanza wa Manase baba ya Gileadi, alikwisha kupewa kwa kura miji ya Gileadi na Basani, maana alikuwa hodari katika vita.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 17:1
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yosefu akamwita mwana wake wa kwanza Manase, akisema: “Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote na jamaa ya baba yangu.”


Mwana wake wa pili akamwita Efuraimu, akisema: “Mungu amenipa watoto katika inchi ya mateso yangu.”


Kule Misri, Asenati binti ya Potifera, aliyekuwa kuhani wa muji wa Oni, alimuzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efuraimu.


Yosefu alipoona kwamba baba yake ameuweka mukono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efuraimu hakupendezwa. Basi, akaushika mukono wa baba yake, akitaka kuuondoa juu ya kichwa cha Efuraimu auweke juu ya kichwa cha Manase.


Akamwambia baba yake: “Sivyo, baba! Huyu hapa ndiye muzaliwa wa kwanza. Tafazali, uweke mukono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”


Yosefu alijaliwa kuwaona watoto na wajukuu wa mwana wake Efuraimu na vilevile kuwapokea kama wana wake watoto wa Makiri mwana wa Manase.


Kule, Abeneri akamusimika Isiboseti kuwa mufalme wa inchi ya Gileadi, Asheri, Yezereheli, Efuraimu na Benjamina na Israeli yote.


Lakini falme za Gesuri na Aramu ziliwashambulia na kuwanyanganya miji ya Yairi, Kenati pamoja na vijiji vyake, jumla ya miji ilikuwa makumi sita. Hao wote walikuwa wazao wa Makiri, baba ya Gileadi.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Hii ndiyo mipaka ya inchi mutakayoigawanyia makabila kumi na mawili ya Waisraeli. Lakini kabila la Yosefu lipewe mara mbili.


Kisha eneo la kabila la Nafutali litafuata eneo la kabila la Manase, kutoka mashariki mpaka magaribi.


Kabila la Manase lilikuwa na jamaa ya: Makiri, Gileadi,


Mala, Noa, Hogla, Milka na Tirsa walikuwa wabinti za Selofehadi. Naye Selofehadi alikuwa mwana wa Heferi mwana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase mwana wa Yosefu.


Basi, Musa akawapa watu wa makabila ya Gadi na Rubeni na nusu ya kabila la Manase mwana wa Yosefu, inchi yote ya mufalme Sihoni wa Waamori na inchi ya mufalme Ogi wa Basani pamoja na miji na maeneo yaliyokuwa kandokando ya miji hiyo.


Anapaswa kukubali yule muzaliwa wa kwanza, mutoto wa yule mwanamuke asiyependwa, na kumupa haki yake: sehemu ya mali zake mara mbili.


Wengine waliobaki wa kabila la Manase walipewa sehemu yao kwa kura kulingana na ukoo zao. Ukoo hizo zilikuwa zile za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Sekemu, Heferi na Semida ambao wote walikuwa wazao wa kiume wa Manase mwana wa Yosefu.


“Murudie kwenu na utajiri mwingi; ngombe wenu wote, feza, zahabu, shaba, chuma na nguo nyingi. Mugawanyane na wandugu zenu vitu vyote mulivyonyanganya kutoka kwa waadui zenu.” Musa alikuwa amepatia nusu ya kabila la Manase sehemu yao kule Basani. Naye Yoshua akaipatia nusu ya pili ya kabila lile sehemu yao kule upande wa magaribi wa muto Yordani kama vile alivyoyapatia makabila yale mengine.


Kutoka Efuraimu waliteremuka katika bonde, wakafuata wandugu zao watu wa Benjamina; kutoka Makiri, majemadari walishuka, kutoka Zebuluni, wenye fimbo ya mutawala.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ