Nyuma ya hayo, kukatokea vita na Wafilistini kule Gezeri. Sibekayi wa muji wa Husati akamwua Sipayi aliyekuwa mumoja kati ya wazao wa majitu; hivyo Wafilistini wakashindwa.
Inchi zao na makao yao yalikuwa: Beteli na vijiji vyake, muji wa Narani uliokuwa upande wa mashariki, muji wa Gezeri uliokuwa upande wa magaribi pamoja na vijiji vyake, Sekemu na vijiji vyake, na Aya na vijiji vyake.
Kutoka kule, mupaka wake ulikwenda kusini kuelekea Luzi kupitia upande wa kusini wa Luzi, ni kusema Beteli, hata Ataroti-Adari, kwenye mulima unaokuwa upande wa kusini wa Beti-Horoni ya Chini.