Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 15:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha, mupaka huo ulipitia kwenye Bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ni kusema Yerusalema, kuelekea kilele cha mulima unaokuwa upande wa magaribi wa bonde la Hinomu na kufika mwisho wa bonde la Refaimu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 15:8
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wafilistini walifika na kujitawanya kwenye Bonde la Refaimu.


Kwa mara ya pili, Wafilistini walifika tena na kujitawanya kwenye bonde la Refaimu.


Mufalme Yosia aliharibu pahali pa kuabudia miungu ya uongo palipoitwa Tofeti katika bonde la wana wa Hinomu, kusudi mutu yeyote asimuteketeze mwana wake au binti yake kama sadaka kwa Moleki.


Nyuma ya hayo Daudi na Waisraeli wote walikwenda Yerusalema, muji uliojulikana kwa jina la Yebusi, na ambao wenyeji wake walikuwa Wayebusi.


akafukiza ubani kwenye Bonde la mwana wa Hinomu na kuwateketeza wana wake kama sadaka, akiiga desturi za kuchukiza za watu ambao walifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Zanoa na Adulamu pamoja na vijiji vilivyoizunguka, Lakisi na mashamba yanayouzunguka, na katika Azeka pamoja na vijiji vinavyouzunguka. Hii ina maana kwamba watu wa Yuda walikaa katika eneo linalokuwa kati ya Beri-Seba upande wa kusini na Bonde la Hinomu upande wa Kaskazini.


Itakuwa kama wakati wa mavuno, wakati wamekwisha kuokota ngano, na kukusanya masuke katika mukono. Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu wakati wamekwisha kuvuna ngano.


Nyuma ya mambo haya, Yeremia aliondoka Tofeti, pahali ambapo Yawe alipomutuma aende kutoa unabii, akaenda kusimama katika kiwanja cha nyumba ya Yawe, akawatangazia watu wote maneno haya:


Halafu uende pamoja nao katika bonde la Mwana wa Hinomu, kwa kupitia mulango unaoitwa mulango wa Vigae. Ukifika huko, utangaze maneno ninayokuambia.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambazo nafasi hii haitaitwa tena Tofeti, wala bonde la Mwana wa Hinomu, lakini itaitwa bonde la Mauaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalema, na mpaka leo Wayebusi wangali wanaishi katika muji ule pamoja na watu wa Yuda.


Kisha ulielekea chini kupitia pembeni ya mulima unaokuwa karibu na bonde la mwana wa Hinomu, ambalo lilikuwa katika sehemu ya kaskazini zaidi ya bonde la Warefaimu. Halafu mupaka uliteremuka kuelekea bonde la Hinomu, upande wa kusini wa kilima cha Wayebusi, ukaendelea kuteremuka mpaka Eni-Rogeli.


Lakini watu wa kabila la Benjamina hawakuwafukuza Wayebusi waliokaa katika Yerusalema; ndiyo maana Wayebusi wanakaa pamoja na watu wa kabila la Benjamina katika Yerusalema mpaka leo.


Watu wa kabila la Yuda waliushambulia Yerusalema na kuuteka. Waliwaua wakaaji wake kwa mapanga na kuuteketeza muji kwa moto.


Lakini yule mutu akakataa kulala kule usiku ule. Basi, akasimama, akaondoka, akafika karibu na muji wa Yebusi, ni kusema Yerusalema. Alikuwa na wale punda wake wawili waliotandikwa tayari, pamoja na habara yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ