Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 15:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Akisa akamujibu: “Unipe zawadi. Unipe sehemu yenye maji kwa sababu kule Negebu ulikonipa ni jangwa.” Basi, Kalebu akamupa chemichemi za maji zilizokuwa upande wa juu na chini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 15:19
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Abramu akaendelea kusafiri kuelekea upande wa Negebu.


Basi, ninakuomba ukubali zawadi niliyokuletea, kwa sababu hata mimi vilevile Mungu amenineemesha, nami nina mali nyingi.” Ndivyo Yakobo alivyomushawishi Esau, naye akapokea zawadi yake.


Ni hivi niliona kuwa ni vizuri kuwashauri wandugu hawa watangulie kufika kwenu mbele yangu kusudi watayarishe vile vitu mulivyoahidi kutoa kwa mapenzi yenu. Hivi vitakuwa tayari na itaonyesha kwamba mumevitoa kwa moyo mwema, wala si kwa uchoyo.


Juu ya kabila la Yuda akasema: “Ee Yawe usikilize kilio cha kabila la Yuda; umurudishe tena kwa wandugu zake. Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake, usaidie kabila la Yuda mbele ya waadui zake.”


Katika siku yao ya arusi, Akisa akamwambia Otinieli amwombe Kalebu shamba. Akisa alikuwa amepanda juu ya punda, na alipokuwa anashuka chini, Kalebu akamwuliza: “Unataka nikupe nini?”


Hii ndiyo inchi watu wa kabila la Yuda waliyopewa kulingana na ukoo zake. Miji iliyokuwa upande wa kusini kabisa wa inchi ya Yuda kuelekea mupaka wa Edomu ilikuwa: Kabuseli, Ederi, Yaguri, Kina, Dimona, Adada, Kedesi, Hazori, Itinani, Zifu, Telemu, Bealoti, Hazori-Hadata, Kerioti-Hesironi (ni kusema Hazori), Amamu, Sema, Molada, Hazari-Gada, Hesimoni, Beti-Peleti, Hazari-Suali, Beri-Seba, Biziotia, Bala, Iyimu, Ezemi, Eltoladi, Kesili, Horma, Ziklagi, Madimana, Sanisana, Lebaoti, Silhimu, Aini na Rimoni. Jumla ya miji makumi mbili na tisa pamoja na vijiji vyake. Miji iliyokuwa kwenye mabonde ilikuwa: Estaoli, Zora, Asina, Zanoa, Eni-Ganimu, Tapua, Enamu, Yarmuti, Adulamu, Soko, Azeka, Sarayimu, Aditaimu, Gedera na Gederotaimu. Jumla ya miji kumi na mine pamoja na vijiji vyake. Zenani, Hadaza, Migidali-Gadi, Dilani, Misipe, Yokiteli, Lakisi, Bozikati, Eguloni, Kaboni, Lamani, Kitilisi, Gederoti, Beti-Dagoni, Nama na Makeda. Jumla ya miji kumi na sita pamoja na vijiji vyake. Libuna, Eteri, Asani, Ifita, Asina, Nesibu, Keila, Akizibu na Maresa. Jumla ya miji tisa pamoja na vijiji vyake. Ekuroni pamoja na miji yake midogo na vijiji, Miji yote na vijiji vilivyokuwa karibu na Asidodi kati ya Ekuroni na bahari, Asidodi na Gaza pamoja na miji na vijiji vyake, mpaka kijito cha Misri mpaka pembeni ya bahari ya Mediteranea. Miji iliyokuwa kwenye eneo la milima ni: Samiri, Yatiri, Soko, Dana, Kiriati-Sana (au Debiri), Anabu, Estemoa, Animu, Goseni, Holoni na Gilo. Jumla ya miji kumi na mumoja pamoja na vijiji vyake. Arabu, Duma, Esani, Yanimu, Beti-Tapua, Afeka, Humuta, Kiriati-Arba (au Hebroni) na Siori. Jumla ya miji tisa pamoja na vijiji vyake. Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta, Yezereheli, Yokidamu, Zanoa, Kaina, Gibea na Timuna. Jumla ya miji kumi pamoja na vijiji vyake. Halihuli, Beti-Zuri, Gedori, Marati, Beti-Anoti na Eltekoni. Jumla ya miji sita pamoja na vijiji vyake. Kiriati-Bali, unaoitwa tena Kiriati-Yearimu, na Raba. Jumla ya miji miwili pamoja na vijiji vyake. Miji ya jangwa ilikuwa: Beti-Araba, Midini, Sekaka, Nibusani, Muji wa Chumvi na Engedi. Jumla ya miji sita pamoja na vijiji vyake.


Bwana wangu, ninakuomba upokee zawadi hii niliyokuletea, na uwape vijana wanaokufuata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ