Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 14:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Siku moja watu wa kabila la Yuda wakamwendea Yoshua kule Gilgali. Kalebu mwana wa Yefune, ambaye alikuwa Mukenizi, akamwambia Yoshua: “Bila shaka unakumbuka jinsi Yawe alivyomwambia Musa, mutu wa Mungu, juu yangu na wewe tulipokuwa Kadesi-Barnea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 14:6
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku moja Yeroboamu alikuwa akisimama pembeni ya mazabahu kusudi afukize ubani. Basi, mutu wa Mungu kutoka Yuda akafika pale Beteli na ujumbe wa Yawe.


Akamufuata yule mutu wa Mungu, akamukuta akiikaa chini ya muti wa mwalo. Basi, akamwuliza: “Wewe ndiwe yule mutu wa Mungu kutoka Yuda?” Naye akamujibu: “Ndiyo. Mimi ndiye.”


Elisha akamwambia: “Mwaka kesho, kwa wakati kama huu, utakuwa na mutoto katika mikono yako.” Mama akamujibu: “Hapana, Bwana wangu! Wewe ni mutu wa Mungu; usinidanganye mimi mutumishi wako!”


Mutu mumoja akatoka Bali-Salisa, akamuletea Elisha mikate makumi mbili iliyotengenezwa kwa shayiri ya malimbuko ya mavuno ya mwaka ule na masuke mabichi ya ngano katika gunia. Elisha akamwagiza Gehazi awape watu wakule.


Mama yule akamwambia mume wake: “Sina shaka kwamba mutu huyu anayefika kwetu kila mara ni mutakatifu wa Mungu.


Halafu Elisha akamukazia macho hata Hazaeli akashikwa na wasiwasi. Kwa rafla, Elisha mutu wa Mungu akaanza kulia.


Kisha Elisha alikwenda Damasiki. Wakati ule mufalme Beni-Hadadi alikuwa mugonjwa na alipoambiwa kwamba Elisha alikuwa Damasiki,


Lakini wana wa Musa, mutu wa Mungu wanatajwa katika kabila la Lawi.


Maombi ya Musa, mutu wa Mungu. Ee Bwana, tangia vizazi vyote, wewe umekuwa usalama wetu.


nikawaleta kwenye nyumba ya Yawe, katika chumba cha wana wa mutu wa Mungu Hanani mwana wa Igidalia. Chumba hicho kilikuwa karibu na chumba cha wakubwa juu ya chumba cha mulinzi wa mulango Maseya mwana wa Salumu.


Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.


Lakini Kalebu akanyamazisha watu mbele ya Musa, akasema: Tuende mara moja tuitwae inchi hiyo. Kwa sababu tuko na uwezo sana wa kushinda.


Lakini kwa sababu mutumishi wangu Kalebu ni tofauti, na amenitii kwa ukamilifu, nitamufikisha kwenye inchi hiyo aliyoingia ndani yake na wazao wake watairizi.


atakayeingia katika inchi hiyo ambayo niliapa kuwapa ikuwe yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.


Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, ambao walikuwa kati ya wale watu waliokwenda kupeleleza hiyo inchi, wakararua nguo zao


Yawe alikuwa amesema kwamba wote watakufia katika jangwa, na kweli hakuna hata mumoja wao aliyebaki muzima, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.


Wote hawataiona, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune wa ukoo wa Kenizi na Yoshua mwana wa Nuni, maana wao wamenitii kwa ukamilifu.


Hii ndiyo baraka ambayo Musa, mutu wa Mungu aliwatakia Waisraeli mbele ya kufa kwake. Alisema hivi:


Hakujatokea tena nabii katika Israeli kama Musa, ambaye Yawe alisema naye uso kwa uso.


Basi, Musa mutumishi wa Yawe akakufa kule katika inchi ya Moabu kulingana na neno Yawe alilosema.


Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


kusudi mutu wa Mungu apate kukamilika na kuwa tayari kabisa kwa kutenda kila kazi njema.


Basi, Yoshua akarudi mpaka katika kambi kule Gilgali pamoja na Waisraeli wote.


Kwa hiyo, muji wa Hebroni ni sehemu yao wazao wa Kalebu mwana wa Yefune Mukenizi mpaka hivi leo, kwa sababu Kalebu alikuwa mwaminifu kwa Yawe, Mungu wa Israeli.


Basi, Otinieli mwana wa Kenazi, ndugu ya Kalebu, akauteka muji huo, naye Kalebu akamupa binti yake.


Waisraeli walivuka muto Yordani katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, wakapiga kambi kule katika muji wa Gilgali, upande wa mashariki wa Yeriko.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ