Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 14:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wazao wa Yosefu walikuwa makabila mawili: Manase na Efuraimu. Kabila la Lawi halikupewa sehemu yoyote ya inchi, lakini miji tu ya kuishi na mashamba ya malisho kwa ajili ya nyama wao na riziki zao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 14:4
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yosefu akamwita mwana wake wa kwanza Manase, akisema: “Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote na jamaa ya baba yangu.”


Mwana wake wa pili akamwita Efuraimu, akisema: “Mungu amenipa watoto katika inchi ya mateso yangu.”


Kule Misri, Asenati binti ya Potifera, aliyekuwa kuhani wa muji wa Oni, alimuzalia Yosefu wana wawili: Manase na Efuraimu.


Nyuma ya mambo hayo, Yosefu akapewa habari kwamba baba yake ni mugonjwa. Hivyo, akatwaa wana wake wawili, Manase na Efuraimu, akakwenda nao kwa baba yake.


Yakobo akaendelea kusema: “Wana wako wawili uliowapata hapa Misri mbele sijafika, ni wana wangu. Efuraimu na Manase watakuwa wangu kama vile Rubeni na Simeoni wanavyokuwa.


Lakini, watoto utakaopata nyuma watakuwa wako, kwa jina la wandugu zao wataitwa katika urizi wao.


Mufalme Hezekia akawatumia ujumbe watu wote wa Israeli na Yuda, na vilevile akawaandikia barua watu wa kabila la Efuraimu na Manase, akiwaalika wote wakuje katika nyumba ya Yawe kule Yerusalema, kusudi wafanye sikukuu ya Pasaka kwa heshima ya Yawe, Mungu wa Israeli.


Kabila la Yosefu baba ya Manase na Efuraimu.


Wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Manase na kabila la Efuraimu, walipewa inchi hiyo kuwa urizi wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ