Mutakapoigawanya inchi kwa kupiga kura kusudi kila kabila lipate sehemu yake, sehemu moja ya inchi ni lazima itakaswe kwa ajili ya Yawe. Urefu wake utakuwa kilometre kumi na mbili na nusu na upana kilometre kumi. Eneo hilo lote litakuwa takatifu.
Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.