Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 14:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Lakini sasa ni muda wa miaka makumi ine na mitano tangu Yawe aliposema na Musa, wakati Waisraeli walipokuwa wanapita katika jangwa. Tangu wakati ule Yawe, kama vile alivyoahidi, amenilinda muzima mpaka leo, na sasa mimi nina umri wa miaka makumi nane na mitano.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 14:10
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wamoja walitangatanga katika jangwa tupu, hawakuweza kufikia katika muji wa kukaa.


Kama watu elfu wakianguka pembeni yako, hata elfu kumi karibu yako, hasara haitakupata.


atakayeingia katika inchi hiyo ambayo niliapa kuwapa ikuwe yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.


Lakini Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, wakabaki wazima kati ya wale watu waliokwenda kupeleleza inchi.


Vita Yoshua aliyopigana na wafalme hawa wote ilikamata muda murefu.


Wakati huu, Yoshua alikuwa muzee wa miaka mingi. Basi, Yawe akamwambia: “Wewe sasa umekuwa muzee wa miaka mingi, na kumebaki bado sehemu kubwa za inchi ambazo hazijatwaliwa.


Lakini bado nina nguvu kama nilivyokuwa wakati ule Musa aliponituma. Hata sasa nina nguvu za kuweza kupigana vita au kufanya kazi nyingine yoyote.


Siku hiyo Musa akaniapia: ‘Hakika sehemu ya inchi ile ambayo ulipita ndani yake itakuwa yako wewe na wazao wako milele. Kwa sababu ya uaminifu wako kwa Yawe, Mungu wako’.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ