Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 13:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Vilevile kuanzia Hesiboni mpaka Ramati-Misipe, Betonimu, na kutokea Mahanaimu hata kwa mupaka wa Debiri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 13:26
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ile nguzo akaiita Misipa, ni kusema “Nafasi ya Ulinzi”, maana alisema: “Yawe akuwe mulinzi kati yako na mimi tunapokuwa mbali bila kuonana.


Daudi alipofika Mahanaimu, alikutwa na Sobi mwana wa Nahasi wa muji wa Raba katika inchi ya Amoni, Makiri mwana wa Amieli wa muji wa Lodebari, pamoja na Barzilayi wa muji wa Rogelimu katika inchi ya Gileadi. Hawa watu waliona kwamba Daudi na watu wake walikuwa na njaa, walikuwa wanachoka na walikuwa na kiu kwa sababu ya kusafiri katika jangwa. Basi, waliwapelekea vitanda, mabeseni, vyombo vya udongo, ngano, shayiri, unga, mihindi yenye kukaangwa, kunde na manjegere, asali, siagi, kondoo na maziwa kutoka nyama wao wa kufugwa.


Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari wa Saulo alikuwa amemukamata Isiboseti mwana wa Saulo na kumupeleka kule Mahanaimu.


Ahabu akawaambia watumishi wake: “Hamujui kwamba muji wa Ramoti-Gileadi ni mali yetu? Mbona basi tunajiikalia tu bila kuunyanganya kutoka kwa mufalme wa Aramu?”


ilikuwa Yazeri, miji yote ya Gileadi na nusu ya inchi ya Waamoni mpaka Aroeri kwa upande wa mashariki wa Raba.


Vilevile miji iliyokuwa katika bonde la Beti-Haramu, Beti-Nimura, Sukoti na Zafoni na inchi yote iliyokuwa ya mufalme Sihoni wa Hesiboni; eneo hilo lilikuwa upande wa mashariki wa Yordani na kupakana na upande wa kusini wa bahari ya Kineroti.


Na ngambo ya muto Yordani, upande wa mashariki wa muji wa Yeriko, walichagua muji wa Bezeri unaokuwa kwenye jangwa katika mabonde ya eneo la kabila la Rubeni. Vilevile wakachagua Ramoti, kule Gileadi ambao ni muji wa kabila la Gadi na Golani kule Basani katika eneo la kabila la Manase.


Katika eneo la kabila la Gadi walipewa Ramoti wa Gileadi, muji wa kukimbilia usalama, pamoja na mbuga zake za malisho, Mahanaimu pamoja na mbuga zake za malisho,


Waamoni wakajikusanya wakapiga kambi yao kule Gileadi. Waisraeli nao wakakusanyika na kupiga kambi yao kule Misipa.


Yefuta akafuatana na wazee wa Gileadi, nao watu wakamufanya kiongozi wao. Yefuta akasema masharti yake kule Misipa mbele ya Yawe.


Kisha roho wa Yawe akamujaza Yefuta, naye akaondoka na kupitia Gileadi na Manase, akarudi Misipa katika inchi ya Gileadi na kuendelea mpaka Amoni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ