Ilipokuwa kwa mwanzo wa mwaka mupya, wakati ambapo wafalme wanaenda kwa vita, Daudi alimutuma Yoabu na wakubwa wake pamoja na waaskari wote wa Israeli kupigana. Nao waliteka Waamoni na kushambulia muji wa Raba. Lakini Daudi alibaki Yerusalema.
Kati ya watu wa ukoo wa Hebroni, Yeria alikuwa kiongozi wa ukoo na jamaa zote, na katika mwaka wa makumi ine wa utawala wa mufalme Daudi, uchunguzi ulifanywa na wanaume wenye uwezo mukubwa wakapatikana kule Yezeri katika jimbo la Gileadi.
Mashamba ya Hesiboni yamefifia, vilevile na zabibu za Sibuma ambazo ziliwalewesha wakubwa wa mataifa. Zikafika Yaweri na kusambaa hata katika jangwa, chipukizi zake zikafika hata ngambo ya bahari.
Ninakulilia wewe muzabibu wa Sibuma kuliko hata watu wa Yazeri. Matawi yako yametanda mpaka ngambo ya bahari ya Chumvi, yakafika hata mpaka Yazeri. Lakini mwangamizaji ameyarukia matunda yako ya wakati wa jua na mizabibu yako.
Kwa hiyo wamevunjika moyo na wengi wanaanguka. Nimeiweka chongo ya upanga katika milango yao yote. Umefanywa uangae kama umeme, umengarishwa kwa ajili ya mauaji.
Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.
Mutaifikia inchi ya Waamoni. Musiwasumbue wala musipigane nao kwa sababu sitawapa sehemu yoyote ya hao wazao wa Amoni ikuwe mali yenu. Hao ni wazao wa Loti, na nimewapa hiyo inchi ikuwe mali yao.’ ”
(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)
Kabila la Gileadi lilibaki ngambo ya Yordani. Kabila la Dani, kwa nini mulibaki ndani ya mashua? Kabila la Aseri lilitulia kule pembeni ya bahari, lilikaa katika kivuko chake.