Walipoikaa kwa kula wakainua macho na kuona kundi la Waisimaeli wakisafiri kutoka Gileadi kwenda Misri. Ngamia wao walikuwa wakibeba ubani, zeri na manemane.
Lakini falme za Gesuri na Aramu ziliwashambulia na kuwanyanganya miji ya Yairi, Kenati pamoja na vijiji vyake, jumla ya miji ilikuwa makumi sita. Hao wote walikuwa wazao wa Makiri, baba ya Gileadi.
Ikiwa watu wa Gadi na wa Rubeni watavuka muto Yordani pamoja nanyi wakiwa na silaha zao chini ya uongozi wa Yawe, mukishinda na kuitwaa inchi hiyo, basi mutawapa inchi ya Gileadi ikuwe mali yao.
Tukateka miji yote katika sehemu za mabonde, za mwinuko, na vilevile eneo lote la Gileadi na Basani mpaka Saleka na Edirei, miji ya mufalme Ogi huko Basani.”
Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.
Wengine walivuka muto Yordani mpaka katika inchi ya Gadi na inchi ya Gileadi. Lakini Saulo alikuwa angali kule Gilgali pamoja na watu wote waliomufuata wakitetemeka.