Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 12:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Utawala wake ulienea mpaka kule kwenye mulima Hermoni, kule Saleka, Basani yote mpaka kwa mipaka ya Wagesuri na Wamakati, nusu ya Gileadi hata kwa mupaka wa inchi ya mufalme Sihoni wa Hesiboni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 12:5
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Abusaloma alikimbilia kwa Talmayi mwana wa Amihudi, mufalme wa muji wa Gesuri. Mufalme Daudi akamufanyia mwana wake Amunoni kilio kwa siku nyingi.


Maana, mimi mutumishi wako, nilipoishi kule Gesuri katika inchi ya Aramu, nilimufanyia Yawe kiapo nikisema kama Yawe akinirudisha Yerusalema basi, nitamwabudu yeye.”


Elifeleti mwana wa Ahasibayi wa Maka; Eliamu mwana wa Ahitofeli wa Gilo;


Kiliabu muzaliwa wake wa pili, mama yake alikuwa Abigaili mujane wa Nabali wa muji wa Karmeli; Abusaloma muzaliwa wake wa tatu, mama yake alikuwa Maka binti ya Talmayi mufalme wa Gesuri;


Kisha wakubwa wote wa waaskari pamoja na watu wao waliposikia kwamba mufalme wa Babeli alimuchagua Gedalia kuwa mutawala, wakamwendea Gedalia kule Mispa. Watu hao walikuwa ni: Isimaeli mwana wa Netania, Yohana mwana wa Karea, Seraya mwana wa Taumeti wa muji wa Netofati, na Yazania mwana wa Mumakati.


Kabila la Gadi lilikuwa na mupaka na kabila la Rubeni upande wa kaskazini, katika inchi ya Basani iliyoenea upande wa mashariki mpaka Saleka.


walimwendea Gedalia kule Misipa. Watu hao walikuwa Isimaeli mwana wa Netania, Yohana na Yonatani wana wa Karea, Seraya mwana wa Tanumeti, nao wana wa Efai kutoka muji Netofa, na Yezania wa muji wa Makati; wote pamoja na watu wao.


Yairi, mutu wa kabila la Manase, alitwaa eneo lote la inchi ya Argobu, ni kusema Basani, mpaka kwenye mupaka wa Gesuri na Maka. Vijiji vyote alivipa jina lake, na mpaka leo vinajulikana kama vile ‘Vijiji vya Yairi’.


Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.


Hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kunyanganya inchi yao yote iliyokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani kutokea bonde la muto Arnoni mpaka kwenye mulima Hermoni na inchi yote ya Araba upande wa mashariki:


pamoja na inchi za Gileadi, eneo la Wagesuri na Wamakati mulima wa Hermoni na inchi yote ya Basani mpaka Saleka;


Katika muda huo, Daudi na watu wake waliwashambulia Wagesuri, Wagirzi na Waamaleki, ambao walikuwa wenyeji wa inchi hiyo tangu zamani. Aliwashambulia katika inchi yao mpaka Suri, hata kwa mupaka na Misri.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ