Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.
Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi– kweli adui anakuja kuwashambulia: ni hakika kama vile Tabori unavyokuwa mulima, kama vile mulima Karmeli unavyoonekana kutoka katika bahari.
Kutokea kule mupaka wake ulikwenda upande wa magaribi hata Marali, ukapitia pembeni ya Dabeseti na kwenda kwenye kijito kinachokuwa upande wa mashariki wa Yokinamu.
Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.
Katika eneo la kabila la Nafutali walipewa Kedesi, muji wa kukimbilia usalama unaokuwa kule Galilaya pamoja na mbuga zake za malisho, Hamoti-Dori pamoja na mbuga zake za malisho na Kartani pamoja na mbuga zake za malisho. Kwa jumla, miji mitatu.
Walawi wengine waliobaki, ni kusema wazao wa Merari, walipewa miji katika eneo la kabila la Zebuluni. Nayo ni Yokinamu pamoja na mbuga zake za malisho, Karta pamoja na mbuga zake za malisho,
Kulikuwa mutu mumoja kule katika muji wa Maoni ambaye alikuwa na biashara ya kondoo katika muji wa Karmeli. Kule Karmeli alifuga kondoo wake na kuwakata manyoya. Alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja.