Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hawa ndio wafalme ambao Waisraeli waliwashinda na kunyanganya inchi yao yote iliyokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani kutokea bonde la muto Arnoni mpaka kwenye mulima Hermoni na inchi yote ya Araba upande wa mashariki:

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 12:1
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni kama umande wa mulima Hermoni, unaoanguka juu ya vilima vya Sayuni! Kutoka huko Yawe anatoa baraka, ndio uzima wa milele.


Akakamata inchi zao kuwa urizi wa watu wake. Wema wake unadumu milele.


Mbingu ni zako na dunia ni yako pia; ni wewe uliyeumba ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka, wakiwa wamefukuzwa kutoka chicha zao, ndivyo wabinti wa Moabu wanavyokuwa kwenye vivuko vya Arnoni.


Kutoka huko wakasafiri, wakapiga kambi upande wa kaskazini wa muto Arnoni, ambao unatiririka kutoka katika inchi ya Waamori na kupitia katika jangwa. Muto Arnoni ulikuwa mupaka kati ya Wamoabu na Waamori.


Waisraeli wakamupelekea mufalme Sihoni wa Waamori, ujumbe huu:


Lakini Waisraeli wakamwua kwa makali ya upanga, wakatwaa inchi yake, tangu muto Arnoni mpaka muto Yaboki, mpaka inchi ya Waamoni; nao mupaka wa inchi ya Amoni ulikuwa unalindwa sana.


Hatutarizi mali yoyote kati yao ngambo ya muto Yordani, kwa sababu sisi tumepata maeneo yetu ngambo hii, upande wa mashariki wa muto Yordani.


Chini ya uongozi wa Yawe, tutavuka na silaha zetu mpaka katika inchi ya Kanana, lakini inchi tuliyopewa hapa upande wa mashariki wa Yordani itakuwa mali yetu.


Basi, Musa akawapa watu wa makabila ya Gadi na Rubeni na nusu ya kabila la Manase mwana wa Yosefu, inchi yote ya mufalme Sihoni wa Waamori na inchi ya mufalme Ogi wa Basani pamoja na miji na maeneo yaliyokuwa kandokando ya miji hiyo.


“Kisha Yawe akatuamuru: ‘Basi! Muanze safari. Muvuke bonde la Arnoni. Mimi nimetia katika mikono yenu Sihoni, mufalme wa Waamori wa Hesiboni na inchi yake. Mushambulie na kuanza kurizi inchi yake.


Kisha Sihoni akatoka na watu wake wote kupigana nasi karibu na muji wa Yahasa.


“Kisha, tukageuka, tukapanda kuelekea Basani. Mufalme Ogi akatoka na watu wake wote kwa kupigana nasi karibu na muji wa Edirei.


wakiwa ngambo ya muto Yordani, katika bonde linalokuwa mbele ya Beti-Peori, katika inchi iliyokuwa ya mufalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala kutoka katika muji wa Hesiboni, ambaye Musa na Waisraeli walimushinda walipotoka Misri.


Inchi hiyo ilienea toka Aroeri kwenye ukingo wa muto Arnoni, mpaka mulima Sirioni, ni kusema Hermoni,


Mutawasaidia mpaka Yawe atakapowapa wandugu zenu vilevile pahali pa kupumzika, kama vile alivyowapa ninyi, nao vilevile warizi inchi ambayo wanapewa na Yawe, Mungu wenu. Kisha mutarudi katika inchi ambayo ni mali yenu na kuirizi, inchi ambayo mulipewa na Musa, mutumishi wa Yawe, ngambo ya muto Yordani.”


aliwateka na kuwaua wafalme wote wa inchi hizo kuanzia kwenye mulima uliokuwa mutupu wa Halaki karibu na Seiri mpaka Bali-Gadi katika bonde la Lebanoni, upande wa kusini wa mulima Hermoni.


Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.


Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu nyingine ya kabila la Manase yalikuwa yamepewa inchi inayokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa, mutumishi wake.


Sasa Yawe, Mungu wenu, amewapa wandugu zenu amani, kama vile alivyoahidi, basi, murudie kwenu katika inchi ambayo mulipewa na Musa mutumishi wa Yawe, ikuwe mali yenu, ni kusema ngambo ya muto Yordani.


Kisha wakasafiri wakipitia katika jangwa kuzunguka inchi ya Edomu na Moabu mpaka walipofika upande wa mashariki wa Moabu, wakapiga kambi ngambo ya muto Arnoni. Lakini hawakuingia katika eneo la Moabu. Muto Arnoni ndio uliokuwa mupaka wa Moabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ