Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 11:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 11:3
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ile nguzo akaiita Misipa, ni kusema “Nafasi ya Ulinzi”, maana alisema: “Yawe akuwe mulinzi kati yako na mimi tunapokuwa mbali bila kuonana.


Lakini wakati malaika aliponyoosha mukono wake kuelekea Yerusalema kwa kuuangamiza, Yawe alibadilisha nia yake. Yawe akamwambia yule malaika aliyetimiza maangamizi kwa watu: “Basi! Inatosha; rudisha mukono wako.” Malaika wa Yawe alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.


na kufika kwenye ukuta wa muji wa Tiro, wakaingia kwenye miji yote ya Wahivi na ya Wakanana. Kisha, walitoka wakaenda Negebu ya Yuda kule Beri-Seba.


Halafu mufalme Asa akatoa tangazo kwa watu wote wa Yuda, bila kumwacha hata mutu mumoja, wahamishe mawe ya Rama na mbao, vifaa ambavyo Basha alivitumia kwa kujenga. Kisha mufalme Asa alitumia vifaa hivyo kwa kujenga kuta za Geba, katika inchi ya Benjamina na Misipa.


Watu wengine wote waliobaki kati ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, maana yake wote hao ambao hawakukuwa wa taifa la Israeli,


Ni kama umande wa mulima Hermoni, unaoanguka juu ya vilima vya Sayuni! Kutoka huko Yawe anatoa baraka, ndio uzima wa milele.


Mbingu ni zako na dunia ni yako pia; ni wewe uliyeumba ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Kuja, muchumba wangu, tuondoke Lebanoni, na tuiache mbali milima ya Lebanoni. Shuka toka kilele cha mulima Amana, toka kilele cha Seniri na Hermoni, toka mashimo ya simba, toka kwenye milima ya chui.


Mimi nitakaa Misipa nipate kuwa musimamizi wenu mbele ya Wakaldea watakaofika kwetu; lakini ninyi muvune matunda na mukamue divai na mafuta, mujiwekee akiba ya vitu hivyo, mukae katika miji mutakayoirizi.


Kisha Yeremia akaenda Misipa kwa Gedalia mwana wa Ahikamu, akakaa naye pamoja na wanainchi waliobaki katika inchi.


Basi, watu hao wote ambao Isimaeli alikuwa amewakamata mateka kutoka Misipa, waligeuka, wakarudi nyuma, wakamwendea Yohana mwana wa Karea.


Isimaeli aliwaua vilevile Wayuda wote waliokuwa pamoja na Gedalia huko Misipa na waaskari Wakaldea waliokuwa pahali pale.


Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.


Inchi hiyo ilienea toka Aroeri kwenye ukingo wa muto Arnoni, mpaka mulima Sirioni, ni kusema Hermoni,


“Yawe, Mungu wenu atawafikisha kwenye inchi ambayo mutakwenda kufanya makao yenu na atafukuza mataifa mengi kutoka inchi hiyo. Mutakapoingia, atafukuza mbele yenu mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi: Wahiti, Wagirgasi, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.


aliwateka na kuwaua wafalme wote wa inchi hizo kuanzia kwenye mulima uliokuwa mutupu wa Halaki karibu na Seiri mpaka Bali-Gadi katika bonde la Lebanoni, upande wa kusini wa mulima Hermoni.


Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.


pamoja na inchi za Gileadi, eneo la Wagesuri na Wamakati mulima wa Hermoni na inchi yote ya Basani mpaka Saleka;


vilevile eneo la Gebali na Lebanoni upande wa mashariki ya Bali-Gadi chini ya mulima Hermoni mpaka Lebo-Hamati;


Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalema, na mpaka leo Wayebusi wangali wanaishi katika muji ule pamoja na watu wa Yuda.


Yoshua akaendelea kusema: “Sasa mutajulishwa kabisa kwamba Mungu Mwenye Uzima yuko kati yenu na kwamba atawafukuza mbele yenu Wakanana, Wahiti, Wahivi, Waperizi, Wagirgasi na Waamoni, na Wayebusi.


Watu wote wa Israeli, kutokea Dani mpaka Beri-Seba, pamoja na watu wa inchi ya Gileadi, wakakusanyika kule Misipa, mbele ya Yawe.


Kisha wakaulizana: “Kati ya makabila yote ya Israeli kuna kikundi chochote ambacho hakikuhuzuria mukutano uliofanyika mbele ya Yawe?” Walikuwa wamefanya kiapo kwamba mutu yeyote ambaye hatahuzuria mbele ya Yawe kule Misipa anapaswa kuuawa.


Wakataka kujua kama kulikuwa kikundi chochote cha makabila ya Israeli ambacho hakikuhuzuria mukutano mbele ya Yawe kule Mispa. Wakagundua kwamba hakuna mutu yeyote kutoka Yabesi-Gileadi aliyekuja kwenye mukutano ule.


Aliacha mataifa ya watu hawa: wakubwa watano wa Wafilistini, Wakanana wote, Wasidoni na Wahivi waliohamia katika milima ya Lebanoni kutoka mulima Bali-Hermoni mpaka kufikia Hamati.


Basi, Waisraeli waliishi pamoja na Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Samweli aliwaita watu wote wakusanyike mbele ya Yawe kule Misipa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ