Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 11:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Hakuna mutu wa kabila la Anaki ambaye alibakia katika inchi ya Israeli; walibaki wachache tu katika miji ya Gaza, Gati na Asidodi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 11:22
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini kwa mwisho wa mwaka wa tatu, watumwa wawili wa Simei walitoroka, wakaenda kwa Akisi mwana wa Maka, mufalme wa Gati. Habari zilipomufikia kwamba wako Gati,


Nyuma ya hayo, mufalme Daudi aliwashinda na kuwanyenyekeza Wafilistini. Akakamata muji wa Gati pamoja na vijiji vyake vilivyokuwa vya Wafilistini.


Beria na Sema walikuwa kati ya jamaa ambazo zilikuwa zinaishi katika muji wa Ayaloni, na kuwafukuza wenyeji wa Gati. Wana wa Beria walikuwa:


Uzia akaondoka kwa kupigana vita na Wafilistini, akabomoa kuta za miji ya Gati, Yabune na Asidodi. Akajenga miji katika eneo la Asidodi na fasi ingine katika inchi ya Filistia.


Sargoni, mufalme wa Asuria, alimutuma jemadari wake mukubwa kushambulia muji wa Asidodi. Naye akaushambulia na kuuteka.


Filipo akajikuta amekwisha kuwa katika muji Azoto. Kisha akapita katika miji yote akihubiri Habari Njema, mpaka alipofika katika muji Kaisaria.


Waavi walikuwa zamani wakiishi katika vijiji vya kando ya Mediteranea mpaka Gaza. Wakafutori kutoka kisiwa cha Kafutori wakawaangamiza, wakaishi humo pahali pao.)


Watu wenyewe ni warefu na wenye nguvu; ni Waanaki ambao kama vile munavyojua na kama vile mulivyosikia watu wanasema juu yao: ‘Nani anayeweza kuwashambulia?’


Yoshua akawashinda watu wote kutokea Kadesi-Barnea mpaka Gaza, na kutokea Goseni mpaka Gibeoni.


Kalebu alizifukuza kutoka muji huo ukoo tatu za Anaki, ni kusema ukoo wa Sesayi, ukoo wa Ahimani na ukoo wa Talmayi.


Watu wa kabila la Yuda vilevile waliteka miji ya Gaza na eneo lake, Askeloni na eneo lake, na Ekuroni na eneo lake.


Aliacha mataifa ya watu hawa: wakubwa watano wa Wafilistini, Wakanana wote, Wasidoni na Wahivi waliohamia katika milima ya Lebanoni kutoka mulima Bali-Hermoni mpaka kufikia Hamati.


Kutoka kwenye kambi ya Wafilistini, shujaa mumoja anayeitwa Goliati, wa muji wa Gati, alijitokeza. Urefu wake ulikuwa metre tatu.


Nyuma ya Wafilistini kuliteka Sanduku la Mungu, walilibeba kutoka muji wa Ebeni-Ezeri mpaka katika muji wao wa Asidodi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ