Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 11:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Wakati ule, Yoshua akakwenda, akawaangamiza Waanaki waliokuwa wanaishi katika milima kule Hebroni, Debiri, Anabu, inchi yote ya milima ya Yuda na Israeli. Yoshua akawaangamiza watu hao pamoja na miji yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 11:21
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kweli tumedanganyika sana kwa kutambikia huko kwenye vilima, hakika wokovu wa Israeli unatoka kwake Yawe, Mungu wetu.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hata hivyo, enyi watu wangu, kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamori ambao walikuwa wakubwa kama mierezi, wenye nguvu kama miti ya mialo. Niliwaangamiza, matawi na mizizi.


Tuliona majitu huko, wazao wa Anaki. Sisi tulijiona kuwa kama mapanzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona sisi.


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


Walikuwa watu wengi, wenye nguvu na warefu kama vile Waanaki. Lakini Yawe akawaangamiza mbele ya Waamori ambao walitwaa inchi yao wakaishi humo pahali pao.


Watu wenyewe ni warefu na wenye nguvu; ni Waanaki ambao kama vile munavyojua na kama vile mulivyosikia watu wanasema juu yao: ‘Nani anayeweza kuwashambulia?’


Aliweza kuitwaa inchi hii yote kwa sababu Yawe, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.


Niliangalia, nami nikaona farasi mumoja mweupe. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na upindi, akapewa taji. Akatoka akiwa mushindaji na mwenye uwezo wa kuendelea kushinda.


Muji wa Hebroni ukapewa kwa Kalebu kufuatana na maagizo ya Musa. Kalebu akazifukuza kutoka kule ukoo tatu za Anaki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ