Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 11:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 11:20
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.


Hivyo, mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Yawe, kusudi atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu mwana wa Nebati, kwa njia ya Ahiya wa Shilo.


Lakini ilikuwa imepangwa na Mungu kwamba maangamizi yatendeke kwa Ahazia kwa njia hiyo ya kumutembelea Yoramu; kwa sababu alipofika kule, alitoka pamoja na Yoramu kwenda kupigana na Yehu mwana wa Nimusi ambaye Yawe alimuchagua kwa kuangamiza uzao wa Ahabu.


Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa mufalme wa Misri. Mimi nimefanya moyo wake kuwa mugumu na wa wakubwa wake kusudi nipate kuonyesha vitambulisho hivi kati yao,


Basi, Musa na Haruni walifanya maajabu hayo yote mbele ya mufalme wa Misri. Lakini Yawe alifanya moyo wa mufalme kuwa mugumu, akakataa kuwaruhusu Waisraeli waondoke katika inchi yake.


Mimi nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao watawafuatilia katikati ya bahari. Nami nitajipatia utukufu kutokana na kuangamizwa kwa mufalme wa Misri na jeshi lake, magari yake ya vita pamoja na wapanda-farasi wake.


Halafu mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye atawafuatilia. Nami nitajipatia utukufu kwa kumwangamiza yeye na jeshi lake. Halafu Wamisri watatambua kwamba mimi ni Yawe.” Basi, Waisraeli wakafanya hivyo.


Yawe akafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye akawafuatilia Waisraeli ambao walikuwa wameondoka Misri katika uhuru.


Yawe akamwambia Musa: “Utakapofika Misri, uhakikishe kwamba umetenda mbele ya mufalme wa Misri miujiza yote niliyokupa uwezo wa kuifanya. Lakini mimi nitafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hatawaachilia Waisraeli waondoke.


Lakini Yawe akafanya moyo wa mufalme wa Misri kuwa mugumu, naye hakuwasikiliza kama vile Yawe alivyomwambia Musa.


Lakini nimewaacha muishi kwa kuonyesha uwezo wangu. Kwa hiyo dunia yote itatambua kwamba mimi ni nani.


Yawe wa majeshi ameapa: Kama nilivyopanga, ndivyo itakavyokuwa; kama nilivyokusudia, ndivyo itakavyokamilika.


Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.


Basi ni kusema kwamba Mungu anamuhurumia yule anayetaka, na kumufanya mugumu yule anayetaka.


“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.


Muangamize taifa lolote ambalo Yawe, Mungu wenu atalitia katika mikono yenu, wala musilionee huruma. Musiabudu miungu yao, maana jambo hili litakuwa mutego kwenu.


Wazazi wake hawakujua kwamba ule ulikuwa mupango wa Yawe ambaye alikuwa anatafuta njia ya kushambulia Wafilistini. Wakati ule, Wafilistini walikuwa wakiwatawala Waisraeli.


Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ