Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 11:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 aliwateka na kuwaua wafalme wote wa inchi hizo kuanzia kwenye mulima uliokuwa mutupu wa Halaki karibu na Seiri mpaka Bali-Gadi katika bonde la Lebanoni, upande wa kusini wa mulima Hermoni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 11:17
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo alipowaona, akasema: “Hii ni kambi ya jeshi la Mungu!” Kwa hiyo akaita pahali pale “Kambi mbili”.


Mbingu ni zako na dunia ni yako pia; ni wewe uliyeumba ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Sasa muvunje kambi yenu muendelee na safari. Muende kwenye inchi ya milima ya Waamori na maeneo ya inchi jirani katika Araba, kwenye milima na mabonde, huko Negebu na sehemu za pembeni ya bahari. Muende mpaka inchi ya Kanana, na inchi ya Lebanoni, mpaka kwenye ule muto mukubwa Furati.


“Kisha, tukageuka, tukasafiri katika jangwa kwa kupitia njia ya bahari Nyekundu, kama vile Yawe alivyoniambia. Tukatangatanga karibu na mulima Seiri kwa muda murefu.


(Wasidoni wanaita mulima huo Sirioni, nao Waamori wanauita Seniri.)


Yawe alikuja kutoka mulima Sinai, alitutokea kutoka mulima Seiri, aliangaza kutoka mulima Parani. Alitokea kati ya maelfu ya wamalaika, na moto unaowaka katika mukono wake wa kuume.


Atawatia wafalme wao katika mikono yenu. Mutawaua, nao watasahaulika. Hakuna mutu yeyote atakayeweza kuwazuia, mpaka mutakapowaangamiza.


Mipaka ya inchi yenu itakuwa hivi: upande wa kusini ni jangwa, kaskazini ni milima ya Lebanoni, mashariki ni muto ule mukubwa Furati, kupitia inchi yote ya Wahiti mpaka bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.


Vita Yoshua aliyopigana na wafalme hawa wote ilikamata muda murefu.


Vilevile, akapeleka ujumbe kwa Wakanana waliokuwa pande za mashariki na magaribi, kwa Waamori, Wahiti, Waperizi, Wayebusi ambao walikaa katika milima na kwa Wahivi ambao walikaa chini ya mulima Hermoni katika inchi ya Misipa.


vilevile eneo la Gebali na Lebanoni upande wa mashariki ya Bali-Gadi chini ya mulima Hermoni mpaka Lebo-Hamati;


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ