Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.
Kisha, wakauchoma kwa moto muji wa Yeriko na kila kitu kilichokuwa mule isipokuwa feza, zahabu, vyombo vya shaba na vya chuma; hivyo viliwekwa katika hazina ya nyumba ya Yawe.