Yoshua 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Mufalme Yabini wa muji wa Hazori alipopata habari hizo, alipeleka ujumbe kwa mufalme Yobabu wa Madoni, kwa mufalme wa Simuroni na mufalme wa Akisafu,
Haya ni maelezo juu ya mufalme Solomono, jinsi alivyowatumikisha watu kazi za kulazimishwa katika kujenga nyumba ya Yawe, nyumba yake ya kifalme, uwanja wa Milo, na ukuta wa Yerusalema, na vilevile katika kujenga upya miji ya Hazori, Megido na Gezeri.
Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.
Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!
Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.
Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mpaka katika hema ya Yaeli, muke wa Heberi Mukeni. Alifanya hivyo kwa sababu kulikuwa amani kati ya mufalme Asikie wa Hazori na jamaa ya Heberi.
Yawe akawatia katika mikono ya mufalme wa Kanana, jina lake Asikie, ambaye aliishi Hazori. Jemadari wa waaskari wake aliitwa Sisera, mukaaji wa Haroseti-Hagoimu.