Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 10:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Yoshua akawashinda watu wote kutokea Kadesi-Barnea mpaka Gaza, na kutokea Goseni mpaka Gibeoni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 10:41
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

hata eneo la inchi yao likakuwa toka Sidona kuelekea upande wa kusini, kuendelea Gerari mpaka Gaza, na kuelekea upande wa mashariki liliendelea kwa Sodoma na Gomora, Adima na Seboimu mpaka Lasa.


Kule Gibeoni, Yawe alimutokea Solomono katika ndoto usiku, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka nami nitakupa.”


Muji wa Askeloni utaona hayo na kuogopa, nao muji wa Gaza utagaagaa kwa uchungu; hata Ekroni, maana tumaini lake litatoweka. Gaza utapoteza mufalme wake, nao Askeloni hautakaliwa na watu.


Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.


Hivi ndivyo walivyofanya babu zenu nilipowatuma kutoka Kadesi-Barnea kwa kupeleleza inchi.


Kisha utapinda kusini kuelekea mupando wa Akarabimu na kupitia Sini mpaka Kadesi-Barnea, upande wa kusini. Kutoka pale, mupaka utapinda kuelekea kaskazini-magaribi mpaka Hasari-Adari na kupita mpaka Azimoni.


Malaika wa Bwana akamwambia Filipo: “Ujitayarishe na uende upande wa kusini kupitia njia inayotelemuka toka Yerusalema kwenda katika muji Gaza, nayo ni njia watu wasiyozoea kupitia.”


“Basi, kama vile Yawe, Mungu wetu, alivyotuamuru, tukaanza safari yetu kutoka mulima Horebu, tukapita katika lile jangwa kubwa la kutisha munalojua, kwa kufuata njia inayoelekea inchi ya milima ya Waamori. Tulipofika Kadesi-Barnea,


Waavi walikuwa zamani wakiishi katika vijiji vya kando ya Mediteranea mpaka Gaza. Wakafutori kutoka kisiwa cha Kafutori wakawaangamiza, wakaishi humo pahali pao.)


Na Yawe alipowatuma kutoka Kadesi-Barnea, akisema ‘Muende murizi inchi ambayo nimewapatia’, hamukufuata amri ya Yawe, Mungu wenu. Hamukuamini wala hamukutii yale aliyowaambia.


Wakati Yawe alipowatia Waamori katika mikono ya Waisraeli, Yoshua alimwomba Yawe mbele ya Waisraeli wote, akasema: “Wewe jua, simama kimya juu ya Gibeoni, wewe mwezi, katika bonde la Ayaloni.”


Habari hizo zilisababisha hofu kubwa kule Yerusalema kwa sababu muji wa Gibeoni ulikuwa mukubwa sana kati ya miji ya kifalme. Muji huu ulikuwa vilevile mukubwa kuliko Ai na wanaume wake wote walikuwa waaskari hodari sana.


Yoshua aliiteka inchi nzima: sehemu za milima na sehemu zote za kusini, eneo lote la Goseni, inchi ya mabonde, inchi ya Araba, milima ya Israeli na sehemu zake za mabonde;


Hakuna mutu wa kabila la Anaki ambaye alibakia katika inchi ya Israeli; walibaki wachache tu katika miji ya Gaza, Gati na Asidodi.


Siku moja Samusoni akakwenda katika muji wa Gaza, akakutana na kahaba mumoja akalala naye.


Wafilistini wakamukamata, wakamwongoa macho, wakamupeleka Gaza, wakamufunga kwa minyororo ya shaba, na kumulazimisha kufanya kazi ya kusaga unga kule katika kifungo.


Wafilistini walizipeleka zile sanamu tano za zahabu na za majipu kwa Yawe zikiwa sadaka ya malipo ya makosa yao, sanamu moja kwa ajili ya muji mumoja, muji wa Asidodi, muji wa Gaza, muji wa Asikeloni, muji wa Gati na kwa muji wa Ekuroni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ