Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 10:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Basi, Yoshua aliiteka inchi yote; akawashinda wafalme wa sehemu za milima, eneo la Negebu, na sehemu za inchi ya bonde na miteremuko. Hakuacha kitu chochote chenye uzima lakini aliangamiza kila kitu kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 10:40
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mara tu alipoanza kutawala, Basha akawaua watu wote wa jamaa ya Yeroboamu; hakuacha muzima hata mutu mumoja wa jamaa ya Yeroboamu. Hiyo ilikuwa sawa na yale Yawe aliyosema kwa njia ya mutumishi wake Ahiya wa Shilo.


Hivyo, hao wazao wakakuja na kurizi inchi. Ulishinda Wakanana na kuwatia katika mikono yao. Watu wako waliweza kuwatendea vile walivyotaka wafalme na watu wa inchi hiyo.


Yawe amejitambulisha; anatoa hukumu. Waovu wamenaswa kwa matendo yao wenyewe.


Mufanye angalisho musifanye agano na wakaaji wa inchi munayoiendea, maana hiyo itakuwa mutego kati yenu.


Alipowatuma kwenda kupeleleza inchi ya Kanana, Musa akawaambia: Muende kule ngambo Negebu, mpaka kwenye inchi ya milima,


Sasa muvunje kambi yenu muendelee na safari. Muende kwenye inchi ya milima ya Waamori na maeneo ya inchi jirani katika Araba, kwenye milima na mabonde, huko Negebu na sehemu za pembeni ya bahari. Muende mpaka inchi ya Kanana, na inchi ya Lebanoni, mpaka kwenye ule muto mukubwa Furati.


Tukaiteka na kuiharibu miji yake yote, tukaua wanaume na wanawake na watoto. Hatukumwacha mutu yeyote muzima.


Atawatia wafalme wao katika mikono yenu. Mutawaua, nao watasahaulika. Hakuna mutu yeyote atakayeweza kuwazuia, mpaka mutakapowaangamiza.


Wakauteka siku hiyohiyo na kuwaua wakaaji wake wote kama walivyofanya kule Lakisi.


na kuuteka. Wakawaua wakaaji wake wote pamoja na mufalme wao; waliiharibu kabisa miji mingine iliyouzunguka, wakawaua wakaaji wake wote kama walivyofanya kule Eguloni.


Waliuteka muji huo na mufalme wake pamoja na miji mingine yote iliyouzunguka na kuwaangamiza wote waliokuwa ndani yao bila kuacha hata mutu mumoja. Waliutendea muji huo kama walivyoutendea muji wa Hebroni na muji wa Libuna na wafalme wao.


Yoshua aliiteka inchi nzima: sehemu za milima na sehemu zote za kusini, eneo lote la Goseni, inchi ya mabonde, inchi ya Araba, milima ya Israeli na sehemu zake za mabonde;


Inchi hizo zilikuwa pamoja na maeneo ya milima, inchi ya bonde, eneo la Araba, miteremuko ya milima, maeneo ya jangwa, na eneo la Negebu; inchi zilizokuwa za Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Miji ya ukoo za kabila la Benjamina ni: Yeriko, Beti-Hogla, Emeki-Kesisi, Beti-Araba, Zemaraimu, Beteli, Awimu, Para, Ofura, Kefari-Amoni, Ofuni na Geba. Jumla ya miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake. Gibeoni, Rama, Beroti, Misipa, Kefira, Moza, Rekemu, Iripeli, Tarala, Zela, Ha-Elefu, Yebusi, ni kusema Yerusalema, Gibea na Kiriati-Yearimu. Jumla ya miji kumi na mine pamoja na vijiji vyake. Hiyo yote ni sehemu watu wa kabila la Benjamina na ukoo zao waliyopewa.


Muji ule utaangamizwa na kila kitu kinachokuwa mule maana umetolewa kwa Yawe. Rahabu, yule kahaba, ndiye atakayeachwa pamoja na wale ambao wako ndani ya nyumba yake kwa sababu aliwaficha wapelelezi wetu.


Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”


Waisraeli waliteka tu nyama na mali kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua.


Wakamujibu Yoshua: “Tuliambiwa kwamba kwa hakika Yawe, Mungu wenu, alimwamuru mutumishi wake Musa awaangamize wakaaji wote wa inchi hii na kuwapa ninyi inchi hii ikuwe mali yenu. Kwa hivyo, tuliogopea maisha yetu na ndipo tukafanya jambo hili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ