Nyuma ya hayo, kukatokea vita na Wafilistini kule Gezeri. Sibekayi wa muji wa Husati akamwua Sipayi aliyekuwa mumoja kati ya wazao wa majitu; hivyo Wafilistini wakashindwa.
Waefuraimu hawakuwafukuza Wakanana walioishi Gezeri. Wakanana hao waliendelea kukaa kati ya watu wa Efuraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.
Walipewa Sekemu, muji ambao ulikuwa vilevile muji wa kukimbilia usalama, pamoja na mbuga zake za malisho katika inchi ya milima ya Efuraimu, na Gezeri pamoja na mbuga zake za malisho,