32 Naye Yawe akautia muji huo katika mikono ya Waisraeli, wakauteka kisha siku mbili. Waliwaua wakaaji wote wa muji huo kama walivyofanya kule Libuna.
Yoshua akawakatakata Waamaleki.
Kisha yule jemadari aliposikia kwamba mufalme wa Asuria alikuwa ameondoka Lakisi, aliondoka na kumukuta akishambulia muji wa Libuna.
Vilevile, kisha Yawe, Mungu wenu, kuyatia katika mikono yenu, mutayashinda na kuyaangamiza kabisa. Musifanye agano lolote nayo wala musiyahurumie.
Siku hiyo Yoshua alipouteka muji wa Makeda, alimuua mufalme wake na wakaaji wake wote bila kuacha hata mutu mumoja. Alimutendea mufalme wa Makeda kama vile alivyomutendea mufalme wa Yeriko.
Kisha kutoka Libuna Yoshua na Waisraeli wote walikwenda Lakisi, wakauzunguka muji ule na kuushambulia.
Hapo, mufalme Horamu wa Gerezi akaamua kuja kuwasaidia watu wa Lakisi. Lakini Yoshua akamwua pamoja na watu wake wote, hakuacha hata mutu mumoja.
Vilevile aliiteketeza miji ile mingine yote kwa moto na kuwaua wafalme wao wote kama vile Musa, mutumishi wa Yawe, alivyomwamuru.