Hivyo Waedomu wakaasi utawala wa Yuda mpaka sasa. Wakati uleule, vilevile wakaaji wa Libuna nao wakaasi utawala wake kwa sababu Yoramu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa babu zake.
Zedekia alikuwa na umri wa miaka makumi mbili na mumoja alipoanza kutawala. Alitawala kwa muda wa miaka kumi na mumoja akiwa kule Yerusalema. Mama yake aliitwa Hamutali binti wa Yeremia, mukaaji wa muji wa Libuna.
Siku hiyo Yoshua alipouteka muji wa Makeda, alimuua mufalme wake na wakaaji wake wote bila kuacha hata mutu mumoja. Alimutendea mufalme wa Makeda kama vile alivyomutendea mufalme wa Yeriko.
Yawe akautia muji huo pamoja na mufalme wao katika mikono ya Waisraeli, wakawaua wakaaji wake bila kuacha hata mutu mumoja. Walimutendea mufalme wa Libuna kama vile walivyomutendea mufalme wa Yeriko.
Zaidi ya kuwapa wazao wa kuhani Haruni muji wa Hebroni ambao vilevile ulikuwa umetengwa kuwa muji wa kukimbilia usalama, waliwapa miji ya Libuna pamoja na mbuga zake za malisho;
Mutautendea muji wa Ai pamoja na mufalme wake kama vile mulivyoutendea muji wa Yeriko pamoja na mufalme wake. Mali zake pamoja na nyama wake mutakayoteka itakuwa ni mali yenu. Muende muushambulie muji kutoka upande wa nyuma.”
Kisha akamutundika mufalme wa Ai juu ya muti wa tini mpaka magaribi. Lakini jua lilipoanza kutua, Yoshua aliamuru maiti yake iondolewe juu ya muti na kutupwa kwenye mulango wa muji kisha walundike lundo kubwa la mawe juu ya maiti hiyo. Lundo hilo liko kule mpaka leo.