Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba, halafu anakutana na dubu! Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake, na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka.
Nilimwona Yawe akisimama pembeni ya mazabahu, naye akaniamuru: Piga zile nguzo za hekalu mpaka misingi yake itikisike. Uvunje zile nguzo ziwaangukie watu juu ya vichwa. Wale watakaobaki nitawaua kwa upanga; hakuna hata mumoja wao atakayeponyoka, hakuna atakayetoroka.
Lakini ninyi musikae kule, muwafuatilie waadui zenu. Muwapige kutoka upande wa nyuma, wala musiwaache waingie katika miji yao, maana Yawe, Mungu wenu, amewatia katika mikono yenu.”