Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 10:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wakati Yawe alipowatia Waamori katika mikono ya Waisraeli, Yoshua alimwomba Yawe mbele ya Waisraeli wote, akasema: “Wewe jua, simama kimya juu ya Gibeoni, wewe mwezi, katika bonde la Ayaloni.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 10:12
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Abeneri mwana wa Neri, pamoja na watumishi wa Isiboseti mwana wa Saulo, waliondoka Mahanaimu na kwenda Gibeoni.


Hezekia akamujibu: “Ni vyepesi zaidi kivuli kwenda mbele hatua kumi! Basi kirudi nyuma hatua kumi.”


Isaya akamwomba Yawe, naye Yawe akafanya kivuli kirudi hatua kumi kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi.


Isaya akamujibu: “Hiki kitakuwa kitambulisho kwako kutoka kwa Yawe, kwamba Yawe atafanya kama alivyoahidi: Unataka kivuli kiende hatua kumi mbele au nyuma?”


Beria na Sema walikuwa kati ya jamaa ambazo zilikuwa zinaishi katika muji wa Ayaloni, na kuwafukuza wenyeji wa Gati. Wana wa Beria walikuwa:


Zora, Ayaloni na Hebroni. Miji hiyo yenye kuzungukwa kuta iko Yuda na Benjamina.


Anaamuru jua lisipande, anafunika nyota zisiangaze.


Mumusifu enyi jua na mwezi, mumusifu enyi nyota zote zinazoangaza.


Si kwa musemo au kwa maneno; wala hakuna sauti inayosikilika;


Muchana ni wako na usiku ni wako; umeweka mwezi na jua kwenye nafasi zao.


Maana Yawe atasimama kama kule kwenye mulima Perasimu; atawaka hasira kama kule katika bonde la Gebeoni. Atatimiza mupango wake wa ajabu; atatenda kazi yake ya ajabu sana.


Nitafanya kivuli kwenye daraja iliyojengwa na Ahazi, kirudi nyuma hatua kumi. Nacho kivuli kikarudi nyuma hatua kumi.


Mwangaza wako muchana hautatua kama jua, wala mwangaza wako usiku kufifia kama mbalamwezi; maana Yawe ni mwangaza wako milele, nazo siku zako za kuomboleza zitakoma.


Katika mwaka uleule, maana yake mwaka wa ine wa utawala wa mufalme Zedekia juu ya Yuda, katika mwezi wa tano, Hanania, mwana wa Azuri, nabii kutoka muji Gibeoni, alisema nami katika nyumba ya Yawe. Alisema nami mbele ya makuhani na watu wote, akiniambia kwamba


Hata hivyo, enyi watu wangu, kwa ajili yenu, niliwaangamiza kabisa Waamori ambao walikuwa wakubwa kama mierezi, wenye nguvu kama miti ya mialo. Niliwaangamiza, matawi na mizizi.


Siku hiyo, nitalifanya jua litue pa saa sita za muchana, na kuijaza inchi giza wakati wa muchana. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; dunia yote ikae kimya mbele yake.


Jua na mwezi vilikaa kimya katika makao yao, vilipoona mwangaza wa mishale yako ikienda mbio, vilipouona mukuki wako ukimetameta.


Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.


naye amekwenda na kutumikia miungu mingine na kuiabudu, akiabudu jua, mwezi au vitu vingine vya mbinguni nisivyoagiza,


Mufanye angalisho kusudi wakati mutakapoangalia na kuona nyota, vitu vyote vya mbinguni, musivutwe kuviabudu na kuvitumikia. Vitu hivyo Yawe amewaachia watu wengine waviabudu.


Jua likasimama kimya na mwezi ukasimama mpaka taifa la Israeli lilipolipiza kisasi waadui zake. Kama vile ilivyoandikwa katika kitabu cha Yaseri, jua lilisimama kimya katikati ya mbingu, likakatiza safari yake ya kwenda kutua kwa siku nzima.


Ayaloni pamoja na mbuga zake za malisho, na Gati-Rimoni pamoja na mbuga zake za malisho. Jumla ya miji waliyopewa ni mine.


Naye akakufa, akazikwa katika muji wa Ayaloni katika inchi ya kabila la Zebuluni.


Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita, zilifuata njia zao zikapigana na Sisera.


Basi, Samweli akamwomba Yawe, naye akatuma radi na mvua katika siku hiyo. Watu wote wakamwogopa sana Yawe na Samweli.


Siku ile, Waisraeli waliwapiga Wafilistini, tangu Mikimasi mpaka Ayaloni. Wakati huu Waisraeli walikuwa wamechoka kwa sababu ya njaa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ