Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Naye Yawe akawatia hofu kubwa mbele ya Waisraeli ambao waliwaua watu wengi kule Gibeoni wakiwakimbia kwenye njia ya muteremuko wa Beti-Horoni mpaka Azeka na Makeda ambako vilevile waliwaua watu wengi sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 10:10
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliwapiga waadui mishale, akawatawanya; alirusha umeme, akawakimbiza.


Basi, Solomono aliujenga upya muji wa Gezeri. Vilevile alijenga Beti-Horoni wa chini;


Asa pamoja na waaskari wake wakawafuatilia mpaka Gerari, wakawaua Waetiopia wengi sana, hapakubaki hata mumoja, maana walikuwa wamekwisha kushindwa na Yawe pamoja na jeshi lake. Jeshi la Yuda likateka vitu vingi sana.


Wakati uleule, wale waaskari Waisraeli ambao Amazia aliwaacha warudi kwao akiwakataza wasijiunge naye katika vita, wakakwenda na kuishambulia miji ya Yuda, toka Samaria mpaka Beti-Horoni, wakaua watu elfu tatu na kunyanganya vitu vingi.


Yawe alinguruma kutoka mbingu; Mungu Mukubwa akatoa sauti yake.


Kwa mukono wako mwenyewe uliyafukuza mataifa, na mahali pao ukawaikalisha watu wako; uliyaazibu mataifa, na kuwafanikisha watu wako.


ingawa walibaki ndani ya mazizi: sanamu za njiwa zilizotengenezwa na feza, na mabawa yao yanayoangaa zahabu.


Alifukuza mataifa mbele yao, akatoa inchi zao zikuwe mali ya Israeli, akaikalisha makabila ya Israeli katika mahema zao.


Maana Yawe atasimama kama kule kwenye mulima Perasimu; atawaka hasira kama kule katika bonde la Gebeoni. Atatimiza mupango wake wa ajabu; atatenda kazi yake ya ajabu sana.


Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.


wakati waaskari wa mufalme wa Babeli walipokuwa wanaushambulia Yerusalema na vilevile miji ya Lakisi na Azeka, ambayo ilikuwa miji pekee iliyobaki ikizungukwa na kuta.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Yawe, Mungu wenu, atawatia waadui zenu katika mikono yenu na atawafanya wahangaike mpaka waangamie.


Walipokuwa wakiwakimbia Waisraeli kwenye muteremuko wa Beti-Horoni, Yawe akawanyeshea mvua ya mawe makubwa kutoka mbinguni wakiwa katika njia mpaka Azeka hata waliouawa kwa mawe hayo wakakuwa wengi kuliko waliouawa kwa silaha za Waisraeli.


Siku hiyo Yoshua alipouteka muji wa Makeda, alimuua mufalme wake na wakaaji wake wote bila kuacha hata mutu mumoja. Alimutendea mufalme wa Makeda kama vile alivyomutendea mufalme wa Yeriko.


Nyuma ya kutembea kutoka Gilgali usiku kucha, Yoshua akawatokea kwa rafla.


Yawe akawatia katika mikono ya Waisraeli, nao wakawashinda na kuwafukuza mpaka Sidona muji mukubwa na Misirepotaimu, mpaka upande wa mashariki katika bonde la Misipa. Waisraeli wakawapiga na kuwaua wote.


Kisha ukashuka upande wa magaribi katika inchi ya Wayefeleti hata Beti-Horoni ya Chini na Gezeri na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea.


Watu wa kabila la Efuraimu kulingana na jamaa zao walipata sehemu yao ambayo mupaka wake upande wa mashariki ulipita Ataroti-Adari hata Beti-Horoni ya Juu,


Kibusaimu pamoja na mbuga zake za malisho na Beti-Horoni pamoja na mbuga zake za malisho. Jumla ya miji waliyopewa ni mine.


Baraka akafanya mashambulizi, naye Yawe akamukimbiza Sisera na waaskari wake wote mbele ya Baraka kwa upanga. Sisera akatoka katika gari lake, akakimbia kwa miguu.


Baraka akawafuatilia waaskari wale na magari mpaka Haroseti-Hagoimu na kuwaua waaskari wote wa Sisera kwa mapanga. Hakukubaki hata mutu mumoja.


Nyota kutoka mbinguni zilishiriki vita, zilifuata njia zao zikapigana na Sisera.


Kikundi kingine kilielekea Beti-Horoni, na kikundi kingine kikageukia njia inayoelekea bonde la Zeboimu, kuelekea katika jangwa.


Wafilistini walikusanya makundi yao ya waaskari kule Soko, muji unaokuwa katika inchi ya Yuda, tayari kwa vita. Walipiga kambi katika sehemu moja inayoitwa Efesi-Damimu kati ya Soko na Azeka.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ