Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Hakikisha kwamba hautakisahau hata kidogo kitabu hiki cha sheria; lakini kila siku utajifunza kitabu hiki, muchana na usiku, kusudi upate kutimiza yote yaliyoandikwa humu, nawe utastawi na kufanikiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 1:8
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku moja magaribi, Isaka akakwenda kwenye mashamba kwa kufikiri. Basi, akainua macho akaona ngamia wanakuja.


Akamutumikia Yawe kwa uaminifu wakati wa kuishi kwa Zakaria, aliyemufundisha kumutii Mungu. Kwa jinsi alivyomutafuta Mungu, Mungu alimufanikisha.


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Ninafikiri juu ya kanuni zako, na kuangalia njia zako.


Ninapenda sana sheria yako! Ninafikiri juu yake muchana kutwa!


Ninaelewa kuliko walimu wangu wote, kwa sababu ninafikiri juu ya maagizo yako.


Unikinge mimi mutumishi wako na makosa ya makusudi, usikubali hayo yanitawale. Hapo nitakuwa mukamilifu, wala sitakuwa na kosa kubwa.


Nimesimulia habari njema ya ukombozi, mbele ya kusanyiko kubwa la watu. Kama unavyojua, ee Yawe, mimi sikujizuia kuitangaza.


Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu, lakini kwa moyo wako ushike amri zangu.


Yawe anasema: Mimi ninafanya nanyi agano hili: Roho wangu anayekuwa juu yenu, maneno niliyoyaweka katika kinywa chenu, hayataondoka kwenu hata kidogo, wala kwa watoto na wajukuu wenu, tangu sasa na hata milele.


Mutu muzuri anatwaa vitu vizuri toka ndani ya akiba yake nzuri, naye mutu mubaya anatwaa vitu vibaya toka ndani ya akiba yake mbaya.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


“Basi kila mutu anayesikia hayo maneno yangu na kuyashika, anafananishwa na mutu mwenye akili aliyejenga nyumba yake juu ya jiwe.


Lakini Yesu akajibu: “Heri zaidi wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii!”


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


“Anayekubali amri zangu na kuzitii, ni yeye anayenipenda. Baba yangu atamupenda yule anayenipenda, na mimi nitamupenda vilevile na nitajitambulisha kwake.”


Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.


Kwa hiyo mukuwe waangalifu kushika maneno yote ya agano hili kusudi mupate kufanikiwa katika kazi zenu zote.


“Leo, mumesimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi wote viongozi wa makabila, wazee wenu, wakubwa wenu,


Sivyo, lakini neno hili liko karibu nanyi, ndani ya vinywa vyenu na ndani ya mioyo yenu, mupate kulitimiza.


wakati watu wa Israeli wanapokuja mbele ya Yawe pahali pale atakapochagua, mutawasomea watu wote wa Israeli sheria hii.


Musa alipomaliza kuandika maneno ya sheria hiyo tangu mwanzo mpaka mwisho,


Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.


Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.


“Ninyi mukuwe waangalifu mufanye kama vile Yawe alivyowaamuru. Mutimize kila kitu sawasawa.


Habari za Kristo zikae ndani yenu kwa uwingi. Mufundishane na mushauriane kwa hekima. Mumwimbie Mungu kwa moyo wenu wote na kumushukuru kwa zaburi na nyimbo za kiroho.


Ukuwe tu imara na hodari. Ukuwe mwangalifu na kushika sheria yote mutumishi wangu Musa aliyokuamuru. Fuata kila sehemu ya sheria hiyo nawe utafanikiwa popote utakapoenda.


Kisha, Yoshua akawasomea sheria zote, pamoja na baraka na laana kama ilivyoandikwa katika kitabu cha sheria.


Heri wale wanaosafisha kanzu zao, kwa maana watakuwa na haki ya kukula matunda ya muti wa uzima na ya kuingia katika muji ule kwa kupitia kwenye milango.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ