Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Ukuwe tu imara na hodari. Ukuwe mwangalifu na kushika sheria yote mutumishi wangu Musa aliyokuamuru. Fuata kila sehemu ya sheria hiyo nawe utafanikiwa popote utakapoenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 1:7
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Mwana wangu, kama inavyokuwa kawaida kwa viumbe vyote kufa, siku zangu zimekwisha. Ukuwe imara na hodari.


Timiza maagizo ya Yawe, Mungu wako, ufuate njia zake na kushika masharti yake, amri zake, maagizo yake na maamuzi yake kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa. Kwa hiyo, utafanikiwa katika kila jambo unalofanya na kokote unakoenda.


Yosia alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata mienendo yote ya babu yake Daudi; hakuiacha hata kidogo.


Ukiwa mwangalifu, na ukitii masharti na maagizo ambayo Yawe alimwagiza Musa juu ya Israeli, utastawi. Ujipe moyo, ukuwe imara. Usiogope wala usifazaike.


Lakini ninyi mujipe moyo, wala musiregee kwa maana mutapata malipo kwa kazi munayofanya.”


Akamutumikia Yawe kwa uaminifu wakati wa kuishi kwa Zakaria, aliyemufundisha kumutii Mungu. Kwa jinsi alivyomutafuta Mungu, Mungu alimufanikisha.


Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.”


Hatutakuacha tena; utujalie uzima, nasi tutakusifu.


Usigeukie kuume wala kushoto; epusha muguu wako mbali na uovu.


Ninatembea katika njia ya haki; ninafuata sheria ya Mungu.


Akaniambia: Usiogope wewe unayependwa sana, uko salama. Ukuwe imara na hodari. Aliposema nami, nilipata nguvu, nikamwambia: Bwana, umekwisha kuniimarisha; sema kile ulichotaka kusema.


Kisha akamwekea mikono juu ya kichwa na kumupa mamlaka kama vile alivyoagizwa na Yawe.


“Mutii amri zote ninazowaamuru siku hii ya leo, kusudi mupate kuingia na kurizi inchi munayoiendea,


bila kugeuka kuume au kushoto kwa kufuata miungu mingine na kuitumikia.


Kwa hiyo mukuwe waangalifu kushika maneno yote ya agano hili kusudi mupate kufanikiwa katika kazi zenu zote.


“Leo, mumesimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi wote viongozi wa makabila, wazee wenu, wakubwa wenu,


Kisha Musa akamwita Yoshua, akamwambia mbele ya watu wote wa Israeli: “Ukuwe imara na hodari, maana wewe utawaongoza watu hawa kwenda kurizi inchi ambayo Yawe aliwaahidi babu zao, nawe utawapatia wairizi.


Musiongeze chochote katika amri ninazowapa, wala musipunguze kitu. Mushike amri za Yawe, Mungu wenu, ambazo ninawapa.


“Ninyi mukuwe waangalifu mufanye kama vile Yawe alivyowaamuru. Mutimize kila kitu sawasawa.


Nyuma ya kifo cha Musa mutumishi wa Yawe, Yawe alimwambia Yoshua mwana wa Nuni, musaidizi wa Musa:


Hakikisha kwamba hautakisahau hata kidogo kitabu hiki cha sheria; lakini kila siku utajifunza kitabu hiki, muchana na usiku, kusudi upate kutimiza yote yaliyoandikwa humu, nawe utastawi na kufanikiwa.


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Musa mutumishi wa Yawe aliipewa amri hii, naye Musa akamwamuru Yoshua ambaye aliitimiza. Yoshua alitimiza kila jambo Yawe alilomwamuru Musa.


Kwa hiyo, mukuwe imara katika kushika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa, musiyaache hata kidogo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ