Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mipaka ya inchi yenu itakuwa hivi: upande wa kusini ni jangwa, kaskazini ni milima ya Lebanoni, mashariki ni muto ule mukubwa Furati, kupitia inchi yote ya Wahiti mpaka bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 1:4
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Gari moja liliweza kununuliwa kule Misri kwa feza inayopita kilo saba, na farasi mumoja aliweza kununuliwa kwa feza kilo mbili. Wachuuzi wa mufalme walisafirisha magari na farasi hao na kuwauzishia wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.


Daudi akamushinda vilevile Hadadezeri mufalme wa Zoba, inchi iliyokuwa karibu na Hamati, alifanya hivyo wakati alipokuwa akienda kujisimamishia nguzo ya ukumbusho kwenye sehemu za muto Furati.


Vilevile, kwa maana makundi yao ya nyama iliongezeka kwa wingi sana, walisambaa upande wa mashariki mpaka kwenye viingilio vya jangwa lililoenea mpaka kwenye muto Furati.


Wafalme wenye nguvu wamepata kuutawala muji ule pamoja na jimbo la upande wa magaribi wa Furati wakilipisha kodi, malipo ya kuvuka mipaka na mengine.


Mipaka ya inchi yenu itakuwa kutoka bahari Nyekundu mpaka bahari ya Mediteranea na kutoka jangwa mpaka muto Furati. Nitawatia wakaaji wa inchi ile katika mikono yenu, nanyi mutawafukuza wawaondokee.


Sasa muvunje kambi yenu muendelee na safari. Muende kwenye inchi ya milima ya Waamori na maeneo ya inchi jirani katika Araba, kwenye milima na mabonde, huko Negebu na sehemu za pembeni ya bahari. Muende mpaka inchi ya Kanana, na inchi ya Lebanoni, mpaka kwenye ule muto mukubwa Furati.


Kila pahali mutakapokanyaga kwa miguu yenu patakuwa penu. Inchi yenu itaenea kutoka katika jangwa, upande wa kusini, mpaka kwenye milima ya Lebanoni upande wa kaskazini, na kutoka muto Furati upande wa mashariki, mpaka kwenye bahari ya Mediteranea upande wa magaribi.


Ninakuomba nivuke muto Yordani, niione inchi hiyo nzuri upande wa magaribi wa Yordani, hakika, inchi nzuri ya kupendeza ya milima, pamoja na milima ya Lebanoni’.


Sauti ile ikamwambia yule malaika wa sita aliyeshika baragumu hivi: “Uwafungue wale wamalaika wane waliofungwa kwenye muto mukubwa Furati.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ