Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yoshua 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Mutawasaidia mpaka Yawe atakapowapa wandugu zenu vilevile pahali pa kupumzika, kama vile alivyowapa ninyi, nao vilevile warizi inchi ambayo wanapewa na Yawe, Mungu wenu. Kisha mutarudi katika inchi ambayo ni mali yenu na kuirizi, inchi ambayo mulipewa na Musa, mutumishi wa Yawe, ngambo ya muto Yordani.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yoshua 1:15
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Upendo haukosi kuwa na adabu, hautafuti faida yake mwenyewe, haukasiriki upesi, nao hauhesabii mutu ubaya.


Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.


Musaidiane ninyi kubeba mizigo yenu, na hivi mutatimiza sheria ya Kristo.


“Wakati ule niliwapa maagizo haya: ‘Yawe, Mungu wenu amewapa inchi hii upande wa mashariki wa muto Yordani ikuwe mali yenu. Sasa ninyi mashujaa kati ya wandugu zenu, mutwae silaha muvuke muto Yordani mukiwa mbele ya wandugu zenu Waisraeli.


Muwasaidie wandugu zenu Waisraeli mpaka Yawe atakapowajalia watulie pahali pao kama vile nanyi mulivyotulia, ni kusema nao vilevile warizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapatia huko ngambo ya Yordani. Nyuma ya hayo, mutaweza kurudia katika inchi yenu hii ambayo nimewapa ikuwe yenu!’


“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.


Kila mutu asitafute faida yake mwenyewe, lakini atafute faida ya watu wengine.


Nyuma ya kifo cha Musa mutumishi wa Yawe, Yawe alimwambia Yoshua mwana wa Nuni, musaidizi wa Musa:


Wake zenu, watoto wenu na nyama wenu wa kufugwa watabaki katika inchi hiyo ambayo Musa aliwapa, ngambo ya muto Yordani. Lakini wanaume wote hodari wakiwa na silaha watavuka muto na kuwatangulia wandugu zenu.


Wakamujibu Yoshua: “Mambo yote uliyotuamuru tutayafanya, na popote utakapotutuma tutakwenda.


Basi, Yoshua akawaita watu wa kabila la Rubeni, la Gadi na watu wa nusu ya kabila la Manase


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ