Wake zenu, watoto wenu na nyama wenu wa kufugwa watabaki katika inchi hiyo ambayo Musa aliwapa, ngambo ya muto Yordani. Lakini wanaume wote hodari wakiwa na silaha watavuka muto na kuwatangulia wandugu zenu.
Yawe akawapa amani kila pahali katika inchi kama vile alivyowaapia wazee wao. Hakuna adui yeyote aliyesubutu kuwashambulia maana Yawe alikuwa amewatia waadui hao katika mikono yao.