Mufalme Daudi alimuchagua Yeriya na wandugu zake elfu mbili na mia saba, mashujaa na viongozi wa ukoo, kwa kusimamia mambo yote yaliyoelekea Mungu na mufalme Daudi katika sehemu za watu wa ukoo wa Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase, zilizokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani.
Makabila ya Rubeni, Gadi na Manase ya upande wa mashariki, yalikuwa na waaskari shujaa yapata elfu makumi ine na ine mia saba na makumi sita, wenye ngao na mapanga, wavuta pinde wafundi katika vita.