Hamani akatoka kule kwenye karamu mwenye furaha tele na moyo mukunjufu. Lakini alipomwona Mordekayi kwenye mulango wa nyumba ya kifalme, hasimami wala hamupi heshima, Hamani akawaka hasira.
Basi, Hezekia aliwakaribisha na kuwaonyesha nyumba alimoweka mali yake: feza, zahabu, viungo vya kukoleza chakula, mafuta ya bei kali, vifaa vyake vyote vya vita na vitu vyote vilivyokuwa katika gala zake. Hakuna chochote katika nyumba yake ya kifalme au katika inchi yake ambacho hakuwaonyesha.
Halafu Yona akatoka inje ya muji, akajiikalia upande wa mashariki wa muji huo. Pale, akajijengea kibanda, akaikaa chini ya kivuli chake akingojea apate kuona jambo litakaloupata muji wa Ninawe.