Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yona 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Halafu Yona akatoka inje ya muji, akajiikalia upande wa mashariki wa muji huo. Pale, akajijengea kibanda, akaikaa chini ya kivuli chake akingojea apate kuona jambo litakaloupata muji wa Ninawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yona 4:5
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Elia aliposikia sauti hiyo, alijifunika uso kwa koti lake, akatoka na kusimama kwenye mulango wa pango. Halafu, akasikia sauti: “Elia! Unafanya nini hapa?”


Kule, akafika kwenye pango, akakaa mule. Mara moja Yawe akamutolea ujumbe: “Elia! Unafanya nini hapa?”


Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao; niliwaazibu, nikauficha uso wangu na kukasirika. Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.


Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.


Watumishi wa mashua wakaogopa, kila mumoja akaanza kumulilia mungu wake. Wakatupa katika bahari mizigo yote kwa kupunguza uzito wa mashua. Wakati ule, Yona alikuwa ameshuka katika sehemu ya ndani ya mashua, akalala usingizi muzito.


Naye Yawe akamujibu Yona: Unazani kwamba unafanya vema kukasirika?


Mungu, Yawe akaamuru mumea uote na kukomaa. Akauotesha kwa kumupatia Yona kivuli cha kumupunguzia taabu aliyokuwa nayo. Yona akaufurahia sana mumea huo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ