Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Yona 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kwa hiyo akaomba: Yawe, si hayo ndiyo mambo yaleyale niliyowaza utayafanya nilipokuwa katika inchi yangu? Ndiyo maana nilifanya haraka kukimbilia Tarsisi. Nilijua kwamba wewe ni Mungu ambaye umejaa huruma na rehema, haukasiriki upesi, wewe ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia yako kusudi usiazibu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Yona 4:2
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”


Yawe ni mwenye rehema na huruma; ni muvumilivu na mwingi wa wema.


Yawe ni mwenye huruma na rehema; yeye hakasiriki upesi, amejaa wema.


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Ee Bwana, wewe ni muzuri na mwenye kusamehe, mwingi wa wema kwa wote wanaokuomba.


Ee Yawe, urudie! Utakasirika mpaka wakati gani? Utuonee huruma sisi watumishi wako.


Basi, Yawe akaacha kuwafanyia watu wake lile jambo baya alilokuwa amesema.


Lakini taifa hilo likigeuka na kuacha uovu wake, basi, mimi nitaacha kulitendea mambo yale niliyokusudia.


Ee Yawe, wewe umenidanganya, nami kweli nimedanganyika; wewe una nguvu kuliko mimi, nawe umeshinda. Nimekuwa mutu wa kuchekelewa kila siku, kila mutu ananizarau.


Sasa basi, mugeuze mienendo yenu na matendo yenu na kutii sauti ya Yawe, Mungu wenu. Mukifanya hivyo, Yawe atabadilisha nia yake na kuacha kuwaletea hasara aliyokusudia kuleta juu yenu.


Kama ninyi mutabaki katika inchi hii, basi, nitawasimamisha, wala sitawaharibu; nitawaotesha wala sitawaongoa; kwa maana nitabadilisha nia kwa sababu ya hasara niliyowatendea.


Basi, Bwana wetu Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Halitatukia!


Basi, Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Hili vilevile halitatukia.


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.


Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


Lakini kwa kutaka kujipatia haki, yeye akamwuliza Yesu: “Mwenzangu ni nani?”


Yawe, Mungu wenu, ni Mungu mwenye rehema, hatawaachilia wala kuwaangamiza, wala kusahau agano ambalo alifanya na wazee wenu kwa kiapo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ